Jumapili, 31 Mei 2015

LIGI YA SODA MUM YA LETA SHANGWE ZA KUFA MTU, YASSIN MKONO NA MWALIM HAMADI NANI NI NANI?

 Baadhi ya Watangazaji wa MUM katika kipindi cha Dimba la michezo wakifuatilia mchezo kati ya  Staff na Mwaka wa pili.

Baadhi ya Wachezaji wa Staff wakijipongeza baada ya kutinga fainali 

 Twalibu chande Mchezaji wa timu ya mwaka wa pili ambaye aligeuka kuwa kocha wa timu ya Staff

Hassan Kimweri miongoni mwa wachezaji wa timu ya Staff akimsaidia Nahodha Mwalim Hamadi baada ya kuumia mchezoni.

 Abrahamani Muchi akitoka kumpisha Mfinanga katika mechi yao dhidi ya Diploma Sayansi.

Mashabiki wa timu ya staff wakimbeba nahodha wa timu hiyo Mwalimu Hamadi baada ya kuibuka washindi na kutinga fainali.

Waliokuwa wanafunzi katika Diploma Sayansi ambao walijitokeza kuwashangilia Sayansi wenzao wakipoteza mchezo dhidi ya staff (Gilbert Jorge kushoto mbele na Kudra Ali kulia mbele)

Mashabiki wakiwa katika Jukwaa la juu kushudia mchezo kati ya staff na diploma sayansi.

 Wadau wa soka wakishuhudia mchezo kati ya Diploma Sayansi na Mwaka wa Tatu katika Uwanja wa chuo Kikuu Cha Waislam Cha Morogoro.

Mashabiki wa soka Chuo Kikuu Cha Waislam cha Morogoro wakishuhudia mechi kati ya Diploma Sayansi na mwaka wa Tatu

Mchezaji Jawadu Juma wa Diploma Sayansi akiwania mpira wakati wa mechi ya nusu fainali ya pili dhidi ya mwaka wa Tatu.


Kikosi cha Timu ya Diploma Sayansi kabla ya mchezo wa nusu fainali dhidi ya mwaka wa tatu.

Kikosi cha Timu ya mwaka wa tatu kabla ya kuingia uwanjani kuwavaa  Diploma Sayansi katika Nusu Fainali ya pili

 Mchezaji wa Timu ya Sayansi Jawadu Juma 'Kinyobwa' akitoka nje ya uwanja akimpisha mchezaji mwenzake kuchukua nafasi yake.

Nahodha wa timu ya wafanyakazi wa chuo(staff)  Mwalimu Hamadi suleiman 'bwana dullah' akikagua mguu wake mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza cha mchezo wao wa kombe la soda chuo kikuu cha waislam cha Morogoro dhidi ya timu ya Diploma Sayansi.

Abdallah Kessy mwamuzi wa michuano ya ligi ya Soda MUM.( picha na Majid Musisy)

Alhamisi, 28 Mei 2015

MWOMBEKI, DAUD 7 MWALIKO WAWAFATA NGASSA,PONDA NA MHANDO BAADA YA KUTOLEWA KATIKA MASHINDANO YA LIGI YA SODA MUM


Timu ya Sayansi MWAKA WA PILI wakipiga jaramba kabla ya nusu fainali yao na Timu ya Staff jion ya leo katika kiwanja cha MUMU( picha na Majid Musisy)


Omary Mwaliko wa kwanza kulia akiongoza benchi la ufundi katika timu ya sayansi Mwaka wa Pili  jioni ya leo dhidi ya Staff MUM. ( picha na Majid Musisy)


Baadhi ya wachezaji wa timu ya Staff wakiwa katika benchi lao wa kwanza kushoto ni Mwl.Malegeri, wa pili Mwl. Chittota, wa tatu kutoka kushoto Mwl. Ferouse. ( picha na Majid Musisy)


Hassan Kimweri mtangazajiwa MUM FM ( aliyesimama) akitathimini nani wa kuziba pengo la Hamed Meena (aliye kaa chini) baada ya kupata jeraha katika nusu fainali ya leo dhidi ya Sayansi Mwaka wa Pili. ( picha na Majid Musisy)




Mwl. Hamad ( timu kaptain ) akiongoza timu yake ya Staff kuelekea mapumziko. ( picha na ( Majid Musisy)


Baadhi ya wachezaji wa timu ya Staff wakiutazama mchezo wao dhidi ya sayansi mwaka wa pili. ( picha na Majid Musisy)


Jumatano, 27 Mei 2015


Rushwa:Maafisa wa Soka wakamatwa Zurich


Waandishi wa Habari wakishuhudia kukamatwa kwa maafisa wa Soka nje ya hoteli mjini Zurich
Maafisa sita wa shirikisho la soka duniani Fifa wamekamatwa katika hoteli moja mjini Zurich,Switzerland. kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Watuhuhumiwa hao ambao wanasemekana kuwa ni pamoja na makamu wa rais wa Fifa,wanashikiliwa wakisubiri kusafirishwa kwenda Marekani.
Shutma hizo zinahusisha rushwa ya takriban kiasi cha dola za Marekani milioni 100 kwa kipindi cha zaidi ya miaka 20
Wanachama wa Fifa wanakutana mjini Zurich kwa ajili ya mkutano wao wa mwaka siku ya ijumaa, ambapo rais wa Shirikisho hilo Sepp Blatter anawania muhula wa tano.
Mwana mfalme Ali Bin Al-Hussein wa Jordan,ambaye ndiye mpinzani pekee wa Blatter amesema tukio hilo ni "baya kwa maendeleo ya soka".
Rais wa Fifa ambaye anawania muhula wa tano ndani ya shirikisho hilo, Sepp Baltter
Gazeti la New York Times limesema askari kanzu walichukua funguo za chumba cha hoteli kutoka eneo la mapokezi ya hoteli ya Baur au Lac hotel ambayo maafisa hao walikuwa wakiishi na kuingia vyumbani mwao.Gazeti hilo limesema Operesheni hiyo ilifanyika kwa utulivu.
Jeffrey Webb, Mkuu wa shirikisho la Amerika ya Kaskazini na Kati na Visiwa vya Caribbean ametajwa kuwa mmoja kati ya maafisa waliokamatwa.
Maafisa wengine wa Fifa walishuhudiwa  wakisindikizwa na Polisi kutoka kwenye hoteli hiyo ni:
Mkuu wa Shirikisho la soka la Costa Rica, Erduado Li, ambaye alikuwa akitarajia kuwepo kwenye mkutano wa kamati ya Fifa siku ya ijumaa.Wengine ni rais wa shirikisho la Uruguay Eugenio Figueredo,rais wa shirikisho la soka Amerika kusini Conmebol na wa Brazil,Jose Maria Marin,mwanakamati ndani ya Fifa,Polisi walionekana wamebeba mikoba yake kwenye mifuko ya Plastiki.
Watu wengi wamekuwa wakijiuliza ni kwa vipi Blatter amekuwa Kiongozi wa Fifa kwa muda mrefu, pamoja na kuwepo kwa ripoti nyingi za vitendo vya rushwa lakini ameendelea kushikilia wadhifa huo.
Wizara ya sheria ya Uswiss imesema katika tamko lake siku ya jumatano kuwa maafisa wa serikali ya Marekani waliwashuku maafisa hao kupokea rushwa ya dola milioni 100, tangu mwanzoni mwa miaka ya 1990 kwa ajili ya michuano ya Amerika ya kati.
Serikali ya Uswiss imesema itaidhinisha haraka kusafirishwa kwao.
Mwanzoni mwa mwezi huu, Blatter alisema anafahamu baadhi ya wafanyakazi wenzake wa zamani walikuwa wakichunguzwa lakini amekanusha kuwa uchunguzi huo ulimhusu pia.

KOCHA MART NOOIJ APUMULIA MASHINE KABLA YA AFCON!!!!!!!

Kufuzu AFCON:Taifa Stars yajiandaa

Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars
Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Mdachi Mart Nooij, amewaita wachezaji 16 kuingia kambini kesho siku ya Jumatano kwa ajili ya kupimwa afya zao na kujua maandeleo yao kabla ya kuwajumUisha katika kikosi cha pamoja kitakachokua kwenye maandalizi ya michuano ya kufuzu ya AFCON 2017 dhidi ya Misri.
Wachezaji walioitwa kuingia kambini kesho ni, Mohamed Hussein, Peter Manyika, Hassan Isihaka, Jonas Mkude (Simba SC), Salum Telela, Juma Abdul, Nadir Haroub (Yanga SC), Aishi Manula, Mudathir Yahya, Frank Domayo, Kelvin Friday (Azam FC), Rashid Mandawa, Atupele Green (Kagera Sugar), Haroun Chanongo (Stand United) Malimi Busungu (Mgambo JKT) na Emmanuel Simwanda (African Lyon).
Mara baada ya kurejea kutoka nchini Afrika Kusini, kocha wa Stars Nooij aliwapa mapumziko ya siku 10, wachezaji waliokua kwenye michuano ya Cosafa mpaka Juni Mosi ambapo ndipo watajumuika na wachezaji wengine waliopo kambini.Tanzania ilifanya vibaya katika michuano hiyo ya Cosafa na kufungwa nan chi zilizochini katika viwango vya chini vya Fifa, Swaziland na Madagascar. Kwa mujibu wa msemaji wa Shirikisho la Soka nchini Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto, ifikapo Juni Mosi, 2015 Taifa Stars itaanza kambi ya moja kwa moja kujiandaa na mechi dhidi ya Misri itakayochezwa jijini Alexandria katika uwanja wa Borg El Arab Juni 14, 2015 ikiwajumuisha pia wachezaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaocheza soka la kulipwa katika klabu ya TP Mazembe ya Congo DR. Kabla ya kuelekea nchini Misri, Taifa Stars inatarajiwa kuweka kambi jijini Addis Ababa nchini Ethiopia kuanzia tarehe 4,Juni 2015 kwa muda wa wiki moja kabla ya kuelekea nchini Misri kwenye mchezo huo dhidi ya Mafarao. Juni 20, 2015 Taifa Stars itawakaribisha Uganda kwenye uwanja wa Aman mjini Zanzibar katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) zitakazofanyika nchini Rwanda 2016, na mchezo wa marudiano kufanyika baada ya wiki mbili nchini Uganda.

Bolt ashinda mita 200

Mwanariadha raia wa Jamaica Usain Bolt ashinda mita 200
Mwanariadha raia wa Jamaica Usain Bolt ameshinda kwa urahis katika shindano lake la kwanza mwaka huu huko barani Ulaya japokuwa ameshindwa kuvunja rekodi yake ya sekunde 20, kwenye mbio za mita 200 za Golden Spike huko Ostrava Jamhuri ya Czech.
Katika shindano hilo lililofanyika jana Bolt alitumia sekunde 20.13 ikiwa ya rekodi yake ya dunia ya sekunde 19.19 akimbwaga mmarekani Isiah Young "huwezi ridhika kama sivunji sekunde 20" alisema Bolt ambaye anajiandaa kwa mashindano ya dunia yatakayofanyika Beijing mwezi August.

Eddie Howe awa meneja bora England

Kocha wa Bournemouth ya England Eddie Howe
Kocha wa timu ya soka Bournemouth ya England Eddie Howe ametajwa kuwa meneja bora wa mwaka wa shirikisho la mameneja wa soka nchini Uingereza LMA.
Kutajwa kwa meneja huyo kunakuja kufuatia kuiongoza kwa mafanikio klabu yake ambayo imeingia ligi kuu ya England kwa mara ya kwanza tokea ianzishwe zaidi ya miaka 100 iliyopita. Howe anakuwa kocha wa pili kutoka nje ya ligi kuu kushinda tuzo hiyo tangia mwaka 1992. "siamini kabisa, ni jambao nisilotarajia" alisema kocha huyo.


MTANI MKUBWA NI MKUBWA, NDO SOKA JIPANGE UPYA

Timu ya Mwaka wa Tatu BAED MUM kabla ya kuminyana na watani wao BAED MWAKA WA PILI juzi uwanja wa MUM (picha na Majid Musisy)


Timu ya MWAKA WA 3 BAED kabla ya kabiliana na watan wao MWAKA WA PILI BAED juzi uwanja wa MUM (picha na Majid Musisy)

Hamis Kawaga ndiye goli kipa bora wa raundi ya kwanza ligi ya Soda MUM kutoka timu ya BAEDB MWAKA WA TATU ( picha na Majid Musisy)

Yasini Mkono aliyefunga goli la pekee kuwaondoa watani wao BAED MWAKA WA PILI katika mashindano ya ligi ya Sonda hapo juzi MUM.( picha na Majid Musisy)

Yasini Mkono akipongezwa na aliye kuwa Waziri wa Usafi na Mazingira katika serikali ya wanafunzi MUM. ( picha na Majid Musisy)

Jumatatu, 25 Mei 2015

Baadhi ya wachezaji wa timu ya Staff ya MUM wakifanya womapu kabla ya mechi yao dhidi ya Wanafunzi wa Mwaka wa pili wakiongozwa na Hamed Meena (wakwanza kushoto) hapo jana kiwanja cha MUM.  (picha na Majid Musisy)



Timu ya wanafunzi wa Mwaka wakwanza kakitroti kabla ya mtanange dhidi ya Timu ya Staff hapo jana katika kiwanja cha MUM. (Picha na Majid Musisy)

Mkono mwamuzi wa mechi ya Staff dhidi ya Mwaka wa Kwanza akifanya ukaguzi kabla ya mchezo kuanza hapo jana katika uwanja wa MUM. ( Picha na Majid Musisy)

Jumamosi, 23 Mei 2015

MAJIDI NA HAMADI DIMBA MAY 23 2015


Baada ya kuchapwa mechi zake zote tatu na kutolewa mapema, timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imewasii salama leo alfajiri ikitokea nchini Afrika Kusini ilipokua ikishiriki michuano ya Kombe la Cosafa,  huku kocha Mart Nooij  akisema amestaajabu.

Stars ambayo jana jioni ilipoteza mchezo wake wa mwisho dhidi ya Lesotho baada ya kufungwa bao 1 - 0, imerejea baadaa ya kupoteza michezo yote mitatu ya kundi B, baada ya kufungwa na Swaziland, Madagascar na Lesotho. 

Mara baada ya mchezo wa jana dhidi ya Lesotho, kocha mkuu wa Taifa Stars Mart Nooij alisema amesikitishwa na matokeo ya timu yake katika hatua hiyo ya awali baada ya kupoteza michezo yote mitatu.
Nooij alisema, mpira wa miguu umebadilika kwani matarajio yake yamekua tofauti, kwani kiwango walivyoonyesha wapinzani wake katika kundi B vimemstajaabisha.
“Mpira wa sasa hautazami nani yupo juu katika renki za FIFA, tulikua na matarajio ya kufanya vizuri katika michuano hii lakini baada ya dakika ya 90 za kila mchezo matokeo hayakua mazuri kwetu” alisema Nooij” 
Kuhusu kufuzu kwa AFCON 2017, Nooij amesema katika kikosi chake alichokwenda nacho Cosafa alikua na wachezaji saba aliowapandisha, anaamini wamepata uzoefu, na sasa atawajumuisha na wachezaji ambao hawakuweza kushiriki michuano hiyo kujiandaa na mchezo dhidi ya Misri.

Taifa Stars inatarajia kucheza kucheza mchezo wake wa kwanza wa kuwania kufuzu kwa AFCON 2017 dhidi ya Misri, tarehe 14 Juni 2015 katika uwanja wa Borg el Arab jijini Alexandria.

Kuhusu kufuzu kwa AFCON 2017, Nooij amesema katika kikosi chake alichokwenda nacho Cosafa alikua na wachezaji saba aliowapandisha, anaamini wamepata uzoefu, na sasa atawajumuisha na wachezaji ambao hawakuweza kushiriki michuano hiyo kujiandaa na mchezo dhidi ya Misri.

Taifa Stars inatarajia kucheza kucheza mchezo wake wa kwanza wa kuwania kufuzu kwa AFCON 2017 dhidi ya Misri, tarehe 14 Juni 2015 katika uwanja wa Borg el Arab jijini Alexandria.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)



KUHUSU MKATABA NA STARS
Mholanzi huyo ataendelea na kazi kwa hoja moja tu ya msingi, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) halina fedha za kumlipa kuvunja naye Mkataba, ambao unamalizika Mei mwakani. 

Kamati ya Utendaji ya TFF itakutana kesho Dar es Salaam kujadili mwenendo wa timu zote za taifa na ajenda kubwa inatarajiwa kuwa Nooij, ambaye katika mechi 16 alizoiongoza Stars tangu awasili mwishoni mwa Aprili kuchukua mikoba ya Mdenmark, Kim Poulsen ameshinda tatu tu, akifungwa sita na sare sita.

Stars imefungwa mechi zote tatu za COSAFA 1-0 na Lesotho jana 2-0 na Madagascar Jumatano na 1-0 na Swaziland Jumatatu.
TFF ilihadaika na wasifu mzuri wa Nooij aliyetua Tanzania akitokea klabu ya St George ya Ethiopia Aprili mwaka jana na kumpa Mkataba mnono. 
Wasifu wa Nooij unasema amewahi kuwa mwalimu maalum katika programu za maendeleo ya soka katika Chama cha Soka Uholanzi (DFA) na pia amewahi kufundisha timu ya EVC 1913 ya Marekani na baadaye Kazakhstan.
Alikuwa kocha wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Burkina Faso katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2003 na mwaka 2004 alikuwa kocha wa muda wa klabu ya FC Volendam ya Uholanzi.
Mwaka 2007 aliteuliwa kuwa kocha wa Msumbiji na akaiwezesha kufuzu kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2010, hiyo ikiwa ni mara ya kwanza Mambas wanashiriki AFCON baada ya msoto wa miaka 12. 
Hata hivyo, katika fainali hizo, Msumbiji ilishika mkia katika kundi lake baada ya kuambulia sare moja na kufungwa mechi mbili. Baada ya kukosa tiketi ya AFCON 2012, Nooij akajiuzulu Septemba mwaka 2011 na nafasi yake kuchukuliwa na Mjerumani, Gert Engels.
Aprili 19 mwaka 2012, aliajiriwa na klabu ya Santos ya Afrika Kusini, ambako hata hivyo alifukuzwa Desemba 18, mwaka 2012 na kuhamia St George ya Ethiopia kabla ya kuja Tanzania Aprili mwaka jana. 
Nooij sasa ataiongoza Stars katika mechi za kufuzu AFCON ikianza na Msiri Juni 13 wakati Julai itakuwa mchezo wa kufuzu CHAN dhidi ya Uganda.


 

 

WABABE WA STARS WATINGA ROBO FAINALI COSAFA, SASA USO KWA USO NA GHANA


MADAGASCAR imetinga robo fainali ya Cosafa baada ya kufanikiwa kumaliza vinara wa kundi B wakiipiku Swaziland kwa idadi nzuri ya magoli ya kufunga na kufungwa.
Timu hizo ambazo zilizokuwa zinachuana kusaka timu moja ya kutinga robo fainali zimetoka sare ya 1-1 usiku huu.
Mechi ya kwanza ya kundi hilo, Madagascar walishinda 2-1 dhidi ya Lesotho, mechi ya pili wakaifumua 2-0 Tanzania ‘Taifa Stars’ na jana wametoka sare ya 1-1 na Swaziland.
Kwa matokeo hayo Madagascar wamefunga magoli 5 na kufungwa 2.
Kwa upande wa Swaziland wao walianza michuano kwa kuifunga 1-0 Taifa Stars, wakashinda 2-0 dhidi ya Lesotho na jana wametoka sare ya 1-1 na Madagascar, hivyo wamefunga magoli 4 na kufungwa 1.
Kwa matokeo hayo, mei 24 mwaka huu Madagascar watacheza mechi ya robo fainali dhidi ya Ghana uwanja wa Moruleng majira ya saa 9:00 kwa saa za Afrika kusini sawa na saa 10:00 kwa saa za Afrika mashariki.
Mechi nyingine ya robo fainali siku hiyo itawakutanisha Malawi na Msumbiji.
Kwa upande wa kundi A, Namibia walifuzu robo fainali na watachuana na Zambia mei 25 mwaka huu uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace majira ya saa 11:30 kwa saa za Sauzi sawa na saa 12:30 kwa saa za Tanzania.
Mechi nyingine ya robo fainali siku ya jumatatu itawakutanisha wenyeji Afrika kusini dhidi ya Botswana.

 

 

NDANDA WADAI CHAO

Licha ya kujituma na kuhakikisha timu yao imebaki katika Ligi Kuu Bara, bado baadhi ya wachezaji wa Ndanda FC wanadai fedha zao za malimbikizo ya mishahara na zile za usajili.


Wakizungumza kwa sharti la kutotajwa, wachezaji hao ambao ni mashujaa kwa kuikoa timu hiyo kuteremka daraja walisema hawaelewi kwa nini hawalipwi fedha zao wakati mara kadhaa Mbunge wa Mtwara Vijijini na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia, amekuwa akitoa fedha.


Alipotafutwa Ofisa Habari wa Ndanda, Idrissa Bandari, alisema: “Kweli tunadaiwa ila hatujui tutawalipa lini hao wachezaji.”

SHERMN ; UKWI MOTO WA KUOTEA MBALI
Straika wa Yanga, Kpah Sherman, ameweka unafiki pembeni na kusema nyota wa Simba, Emmanuel Okwi, kwa jinsi anavyocheza uwanjani, ana uhakika wa kucheza soka popote pale hata nje ya Afrika.

Sherman, raia wa Liberia ambaye alitua Yanga Desemba mwaka jana akitokea Klabu ya Cetinkaya ya Cyprus, amewahi kucheza timu moja na kiungo wa Mtibwa Sugar, Henry Joseph katika kikosi cha Kongsvinger ya Norway.

Sherman amesema Okwi anajua majukumu yake uwanjani na kwa uwezo wake, anaweza kucheza soka la kulipwa popote pale Afrika hata nje ya bara hili.


“Okwi ni rafiki yangu wa karibu, anacheza kwa kujituma sana, anamiliki mpira, anatumia akili nyingi sana uwanjani na vitu vingine vingi, ambavyo naweza kusema anaweza kucheza popote,” alisema Sherman ambaye ameifungia Yanga mabao sita tangu alipojiunga nayo.


Wakati huohuo, Sherman alisema pengo la winga Mrisho Ngassa aliyejiunga na Free State kwa dau la dola 150,000 (Sh milioni 300) katika timu yao, linahitaji mtu makini kuliziba, vinginevyo timu haitakuwa imara.



VURUGU ZA BURUNDI SIMBA NAO NI WAATHIRIKA

  

Simba imeamua kumsubiri mshambuliaji Laudit Mavugo amalize mechi mbili katika kikosi chake cha Vital’O kabla ya kuja kujiunga nayo kwa ajili ya majaribio.


Lakini vurugu za kumpinga Rais Pierre Nkurunziza ambaye anataka kugombea kwa muhula wa tatu, ndizo zimechangia zaidi Simba kufanikisha jambo hilo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe ambaye amekuwa akilifuatilia suala hilo kwa karibu, amekiri vurugu hizo zimechangia kuongeza ugumu wa jambo hilo.

“Kweli hapa kuna suala la kusubiri amalize ligi na zimebaki mechi mbili. Tumefanya mazungumzo na klabu yake, pia imani yangu mambo yatakwenda vizuri.

Mavugo amekuwa tegemeo katika safu ya ushambuliaji wa Vital’O na aliwahi kufanya kazi na Kocha Goran Kopunovic.

Kopunovic ndiye aliyempendekeza Mavugo kwa kuwa alikuwa mchezaji wake akiwa Polisi Rwanda. Lakini mwisho yeye ameondoka baada ya kutaka apewe dau la Sh milioni 100 ili asaini mkataba mpya, jambo ambalo Simba hawakukubaliana naye.

Simba imekuwa haina straika wa uhakika wa ‘kucheka’ na nyavu mara baada ya kumruhusu Amissi Tambwe aondoke.

Tambwe aliondoka Simba akiwa mchezaji huru, Yanga ikaokota ‘dodo’ na sasa ni kati ya wachezaji inaowategemea katika ufungaji.


KIMATAIFA

ADEBAYOR APEWA MDA WA KUSULUHISHA MGOGORO
Mchezajii wa kilabu ya Tottenham Emmanuel Adebayor amepewa mapumziko kwa mara ya pili msimu huu lakini hatma yake katika kilabu ya Spurs haijulikani.
Mchezaji huyo wa taifa la Togo mwenye umri wa miaka 31 ameandika kuhusu matatizo ya famili yake katika mtandao wa facebook na kusema kuwa alikuwa ameamua kujiuua.
Atakosa mechi ya siku ya jumapili kati ya kilabu yake na Everton mbali na ziara ya Kuala Lumpur na baadaye nchini Sidney.
''Tumempa mda wa kusuluhisha mzozo na familia yake'',alisema kocha wa kilabu hiyo Mauricio Pochettino.Ni miasha yakje ya kibinafsi .Niliongea naye mapema wiki hii,ni hali ngumu kwake''.
Adebayor alijiunga na klabu ya Spurs mwaka 2011 kutoka Manchester City kupitia mkopo kabla ya mabao 18 aliyofunga akiwa na Hotspurs kumwezesha kupewa kandarasi ya kudumu.



Kocha msaidizi wa Manchester United Ryan Giggs amesema ni kituko kwa Manchester United kushangilia nafasi ya nne.
Giggs ambaye ameichezea United kwa miaka 27, ameshinda mara 13 taji la Premier League na mataji mawili ya Champions League kama mchezaji.
Baada ya kudondoka kwa timu chini ya David Moyes, hatimaye United ikiwa na Louis van Gaal imejitutumua na kushika nafasi ya nne, jambo linloonekana kama ushindi fulani.
Giggs amekiri kufurahia mafanikio ya Manchester United katika msimu wake wa kwanza kama msaidizi wa Van Gaal lakini akasema msimu ujao ni wa kupigania ubingwa.
Akizungumza katika sherehe za kufunga msimu kwa klabu hiyo ya Old Trafford, Giggs akasema: Inashangaza kwa mtu ambaye umekuwa kwenye klabu hii kwa muda mrefu na kwa mafanikio ya hali ya juu, kusimama na kushangilia nafasi ya nne.
“Lakini sio siri na bila hiyana, hiki ndicho tulichodhamiria wakati msimu uliopokuwa unaanza – kupata nafasi ya kucheza Champions League. Ila msimu ujao tunataka kupigania mataji”.
Manchester United ina uwezekano wa kushika nafasi ya tatu kama itashinda mchezo wake wa mwisho Jumapili na wakati huo huo Arsenal ifungwe.



 REAL MADRID YAWASILIANA NA BENITEZ

Mkufunzi wa kilabu ya Napoli Rafael Benitez ameorodheshwa miongoni mwa makocha wataokumrithi Carlo Ancelotti katika kilabu ya Real Madrid.
Ancelotti anatarajiwa na wengi kuachana na kilabu hiyo baada ya mechi ya mwisho na Getafe wikiendi hii.
Mazungumzo kati ya Real Madrid na Benitez yanaendelea huku kandarasi ya Benitez katika kilabu ya Napoli ikitarajiwa kukamilika mwezi ujao,ijapokuwa hakuna makubaliano yalioafikiwa.
Klabu ya West Ham pia iliwasiliana na kocha huyo ambaye aliwahi kuifunza Chelsea na Liverpool.

Mkufunzi wa West Ham ambaye anaiandaa West Ham dhidi ya Newcastle anatarajiwa kuanzisha mazungumzo na klabu hiyo kuhusu hatma yake wiki ijayo.
Benitez alianza kazi ya ukufunzi katika kilabu ya Real Madrid B na pia amewahi kuifunza Valladolid,Osasuna,Etramadura,TenerifeValencia na Inter Milan.




Wakati tetesi za Carlo Ancelotti kuwa kikaangoni Santiago Bernabeu zikizidi kusambaa, wakala wa Rafael Benitez amefichua kuwa mteja wake atafurahia nafasi ya kuikochi Real Madrid.

Kwa mujibu wa gazeti la Marca la Hispania, kocha huyo wa Napoli hana mpango wa kusaini mkataba mpya kwa miamba hiyo ya Serie A huku habari zikisema ni mmoja wa makocha wanaowaniwa na Real  Madrid kuziba nafasi ya Carlo Ancelotti.

Kama vile hiyo haitoshi, inasemekana mmiliki wa AC Milan Silvio Berlusconi naye anamtaka Carlo Ancelotti arejee nyumbani kuikochi timu hiyo.

Benitez amewahi kuhusishwa na Real Madrid mara kadhaa huko nyuma hasa baada ya kuipa Valencia mataji mawili ya La Liga na pale alipoiwezesha Liverpool kutwaa kombe la Champions League.

Akiongea na kituo cha TV cha Cuatro, wakala wa Benitez, Manuel García Quilón alisema: “Huu ni uvumi wa nguvu sana, hakuna maongezi yoyote mpaka muda huu, lakini mteja wangu atafurahia nafasi hiyo.
“Rafa alikuwa mchezaji wa Real Madrid, akawa kocha wa vijana klabuni hapo na anatokea Madrid – ni nani ambaye hatafurahishwa na nafasi hiyo?

“Sipo ndani ya kichwa chake, lakini najaribu kuvuta picha na kuona ni jinsi gani atafurahia mafasi hiyo”.

Bosi wa Napoli Rafa Benitez anatarajiwa kuanza maongezi na rais wa Real Madrid, Florentino Perez kwaajili ya kurejea Santiago Bernabeu
      



Bottom of Form


Manchester City inatajwa kuwa iko kwenye nafasi nzuri zaidi ya kumtwaa Raheem Sterling wa Liverpool pindi dirisha la usajili litakapo funguliwa mwezi ujao.
City ipo tayari kulipa pauni milioni 45 kwa  winga huyo wa kimataifa wa England sambamba na mshahara wa pauni 120,000 kwa wiki.
Hata hivyo kocha wa City Manuel Pellegrini amesema kwa sasa hawezi kuongea chochote kuhusu Sterling: “Sijui nini kitatokea kwa Raheem, kuna wachezaji wengi muhimu ambao kila klabu ingependa kuwa nao.
“Tunamaliza msimu kesho na baada ya hapo tutaangalia ni wachezaji gani wa kuwaleta klabuni kwetu.
“Hakutakuwa na mabadiliko makubwa sana kwa sababu sidhani kama tunahitaji kufanya hivyo. Tutajitahidi kuwa na kikosi imara kila mwaka, sio kwasababu tumekosa taji msimu huu, bali ni kwasababu ni muhimu kufanya mabadiliko yenye tija kila mwaka.”


Bottom of Form

Kama wanasheria wa Barcelona watafanikiwa kutengua adhabu ya klabu kufungiwa usajili, basi biashara ya kwanza itakuwa ni kwa kiungo wa Arsenal, Aaron Ramsey (pichani juu kulia).
Barcelona inataka kumnunua Ramsey – Arsenal inaweza kuwa chimbo la kuineemesha Barcelona kwa mara nyingine tena.
Pauni milioni 50 zinatajwa kuwa ndio kiasi kinachoandaliwa na Barcelona kwaajili ya nyota huyo kimataifa wa Wales, wakitaraji kumchukua mchezaji wa tisa kutoka Arsenal kuanzia mwaka 2000.
Barcelona wapo kwenye kifungo cha kusajili lakini wana matumaini ya kuachiwa huru katika dirisha la kiangazi na iwapo kama hilo halitafanikiwa basi watakomaa na Ramsey katika dirisha la Januari pale adhabu yao itakapokuwa imeisha.