Yanga yashinda, Azam yavutwa shati
![]() |
Wanajagwani wakishangilia ushindi dhidi ya Kagera Sugar jana taifa |
Ligi kuu ya Tanzania bara iliendelea tena mwisho wa wiki kwa michezo mitano kupigwa.
Katika dimba la Taifa Jijini Dar Es Salaam klabu ya soka ya Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Kagera Sugar.Mabao ya wanajangwani hao yalifungwa na Donald Ngoma, Amisi Tabwe na mlinzi wa kushoto haji Mwinyi akifunga bao la mwisho,huku bao pekee la Kagera Sugar likifungwa na Mbaraka Yussuf.
Nao Azam Fc wakicheza ugenini kwenye dimba la Kirumba huko Mkoani Mwanza walikwenda sare ya bao 1-1 na Toto Africans.
Matokeo ya michezo mingine ni
Stand United 2 – 0 Mgambo JKT
Ndanda FC 0 – 0 Tanzania Prisons
JKT Ruvu 1 – 0 African Sports
source bbc swahil
YANGA WAENDA KUIWEKEA KAMBI PEMBA AL AHLY
Kikosi cha watoto wa Jangwani Yanga. |
Wachezaji wote wa Yanga akiwemo Haruna Niyonzima ambaye anasumbuliwa na Malaria na pia hatacheza mechi ya kwanza dhidi ya Al Ahly kutokana na kuwa anatumikia adhabu ya kadi za njano wanasafiri kwa ndege leo.
Kikosi cha Yanga kinachotarajiwa kuingia kambini leo ni makipa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Deo Munishi ‘Dida’ na Benedicto Tinocco.
Mabeki ni Juma Abdul, Oscar Joshua, Mwinyi Hajji Mngwali, Pato Ngonyani, Kevin Yondan, Vincent Bossou (Togo) na Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
Viungo ni Salum Telela, Mbuyu Twite (DRC), Said Juma ‘Makapu’, Thabani Kamusoko (Zimbabwe), Haruna Niyonzima (Rwanda), Simon Msuva, Deus Kaseke, Godfrey Mwashiuya na Issoufou Boubacar (Niger).
Washambuliaji ni Paul Nonga, Matheo Anthony, Malimi Busungu, Amissi Tambwe (Burundi) na Donald Ngoma (Zimbabwe).
Benchi la Ufundi ni Kocha Mkuu, Hans van der Pluijm (Uholanzi), Kocha Msaidizi, Juma Mwambusi, Kocha wa makipa, Juma Pondamali
Daktari, Edward Bavu, Mchua Misuli, Jacob Onyango, Mtunza Vifaa, Mohammed Mpogolo na
Meneja; Hafidh Saleh.
source bin zubery
KIMATAIFA
Jedwali la msimamo wa ligi ya EPL
EPL kufikia 4 Aprili, 2016.
Nambari | Klabu | Mechi | Mabao | Alama |
1 | Leicester | 32 | 24 | 69 |
2 | Tottenham | 32 | 32 | 62 |
3 | Arsenal | 31 | 22 | 58 |
4 | Man City | 31 | 24 | 54 |
5 | Man Utd | 31 | 12 | 53 |
6 | West Ham | 31 | 12 | 51 |
7 | Southampton | 32 | 8 | 47 |
8 | Stoke | 32 | -3 | 47 |
9 | Liverpool | 30 | 5 | 45 |
10 | Chelsea | 31 | 8 | 44 |
11 | West Brom | 31 | -7 | 40 |
12 | Everton | 30 | 9 | 38 |
13 | Bournemouth | 32 | -16 | 38 |
14 | Watford | 31 | -6 | 37 |
15 | Swansea | 32 | -9 | 37 |
16 | Crystal Palace | 31 | -8 | 34 |
17 | Norwich | 32 | -21 | 31 |
18 | Sunderland | 31 | -19 | 27 |
19 | Newcastle | 31 | -27 | 25 |
20 | Aston Villa | 32 | -40 | 16 |
source bbc swahil
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni