Jumatatu, 4 Aprili 2016





Yanga yashinda, Azam yavutwa shati
Wanajagwani wakishangilia ushindi dhidi ya Kagera Sugar jana taifa


              
Ligi kuu ya Tanzania bara iliendelea tena mwisho wa wiki kwa michezo mitano kupigwa.
Katika dimba la Taifa Jijini Dar Es Salaam klabu ya soka ya Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Kagera Sugar.
Mabao ya wanajangwani hao yalifungwa na Donald Ngoma, Amisi Tabwe na mlinzi wa kushoto haji Mwinyi akifunga bao la mwisho,huku bao pekee la Kagera Sugar likifungwa na Mbaraka Yussuf.
Nao Azam Fc wakicheza ugenini kwenye dimba la Kirumba huko Mkoani Mwanza walikwenda sare ya bao 1-1 na Toto Africans.


Matokeo ya michezo mingine ni
Stand United 2 – 0 Mgambo JKT
Ndanda FC 0 – 0 Tanzania Prisons
JKT Ruvu 1 – 0 African Sports
source bbc swahil




Kikosi cha watoto wa Jangwani Yanga.


Wachezaji wote wa Yanga akiwemo Haruna Niyonzima ambaye anasumbuliwa na Malaria na pia hatacheza mechi ya kwanza dhidi ya Al Ahly kutokana na kuwa anatumikia adhabu ya kadi za njano wanasafiri kwa ndege leo.

Kikosi cha Yanga kinachotarajiwa kuingia kambini leo ni makipa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Deo Munishi ‘Dida’ na Benedicto Tinocco.

Mabeki ni Juma Abdul, Oscar Joshua, Mwinyi Hajji Mngwali, Pato Ngonyani, Kevin Yondan, Vincent Bossou (Togo) na Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
Viungo ni Salum Telela, Mbuyu Twite (DRC), Said Juma ‘Makapu’, Thabani Kamusoko (Zimbabwe), Haruna Niyonzima (Rwanda), Simon Msuva, Deus Kaseke, Godfrey Mwashiuya na Issoufou Boubacar (Niger).

Washambuliaji ni Paul Nonga, Matheo Anthony, Malimi Busungu, Amissi Tambwe (Burundi) na Donald Ngoma (Zimbabwe). 

Benchi la Ufundi ni Kocha Mkuu, Hans van der Pluijm (Uholanzi), Kocha Msaidizi, Juma Mwambusi, Kocha wa makipa, Juma Pondamali
Daktari, Edward Bavu, Mchua Misuli, Jacob Onyango, Mtunza Vifaa, Mohammed Mpogolo na 
Meneja; Hafidh Saleh. 



source bin zubery




KIMATAIFA


Jedwali la msimamo wa ligi ya EPL


EPL kufikia 4 Aprili, 2016.
NambariKlabuMechiMabaoAlama
1Leicester322469
2Tottenham323262
3Arsenal312258
4Man City312454
5Man Utd311253
6West Ham311251
7Southampton32847
8Stoke32-347
9Liverpool30545
10Chelsea31844
11West Brom31-740
12Everton30938
13Bournemouth32-1638
14Watford31-637
15Swansea32-937
16Crystal Palace31-834
17Norwich32-2131
18Sunderland31-1927
19Newcastle31-2725
20Aston Villa32-4016






source bbc swahil

Hakuna maoni: