
Blatter aliyekuwa ameudhika sana na tukio hilo alisema 'halikuhusiana kwa njia yeyote na kandanda' kabla yake kuondoka ukumbini.
Blatter alitangaza mabadiliko kadha ikianza na tarehe ya uchaguzi ambayo itakuwa mwezi Februari mwakani.

Rais wa shirikisho la soka barani Ulaya (Uefa) Michel Platini, anadaiwa kupata shinikizo kutoka kwa viongozi wengi wa bara hilo kuwasilisha ombi lake la kuwa rais wa FIFA.
Mkutano huo wa leo pia ulitaja baadhi ya mambo yatakayorekebishwa ikiwa ni pamoja na kuweka kikomo cha muhula cha urais na viongozi wengine wa ngazi ya juu wa shirikisho hilo.

Aidha FIFA itateua jopo la watu 11 watakaoanza uchunguzi wa kina kubaini njia za kukabiliana na rushwa na ubadhirifu.
Jopo hilo maalum ndilo litakaloendesha mabadiliko katika Fifa.
(chanzo bbcswahili.com)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni