Jumamosi, 27 Juni 2015

KAMATI YA TFF YAKUTANA, SUALA LA SIMBA, MESSI BADO PASUA KICHWA, SASA HADI WIKI IJAYO



Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
MABINGWA wa Tanzania Bara, Yanga SC jioni ya leo wamelazimishwa sare ya bila kufungana na SC Villa ya Uganda katika mchezo wa kirafiki, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga SC watajilaumu wenyewe kwa sare hiyo, kwani walipata nafasi kadhaa za kufunga ikiwemo penalti, iliyopaishwa na mchezaji bora wa Ligi Kuu, Simon Msuva dakika za lala salama.
Timu hizo zilianza kushambuliana kwa zamu, huku zote zikicheza soka maridadi ya utulivu na pasi za uhakika kabla ya dakika ya 27 Kasumba Omary wa Villa nusura kumzunguka Nahodha wa Yanga SC, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ lakini beki wa kulia Oscar Joshua akaondosha mpira kwenye hatari.
Dakika ya 28 Achema Robert alipiga shuti kali likatoka nje, kabla ya shuti lake lingine kudakwa na kipa wa Yanga SC, Ally Mustafa ‘Barthez’ dakika ya 33.
Malimi Busungu wa Yanga SC alipiga nje dakika ya 32 kufuatia pasi nzuri ya Amisi Tambwe. Busungu tena dakika ya 35 alimdakisha kipa wa Villa, Sebwato Nicolaus baada ya kupiga ndani ya boksi.
Tambwe naye alipoteza nafasi ya kufunga dakika ya 34 baada ya shuti lake kudakwa na kipa wa Villa, Sebweto.
Katika mchezo huo, Kocha mpya wa Simba Dylan Kerr aliingia kuwatazama wapinzani, kipindi cha pili Yanga SC walitengeneza nafasi nzuri, lakini wakashindwa kutumia.
Dakika ya 50 Deus Kaseke aligongesha mwamba, dakika ya 54 krosi nzuri ya Juma Abdul ilidakwa na kipa wa Villa, Sebwato.
Yanga SC ilipata pigo dakika ya 71, baada ya Nahodha wake, Cannavaro kuumia juu ya jicho na kushindwa kuendelea na mchezo, nafasi yake ikichukuliwa na Pato Ngonyani aliyekwenda kucheza vizuri.
Winga mpya machachari wa Yanga SC, Godfrey Mwashiuya aliunganisha vizuri krosi ya Kpah Sherman dakika ya 76, lakini beki wa Villa, Wasibi akaokoa mpira ukiwa unaelekea nyavuni.
Msuva akapaisha penalti dakika ya 78 baada ya kipa wa Villa kumuangusha Kaseke kwenye eneo la hatari na dakika ya 80 Mwashiuya aliipiga shuti maridadi lililookoleea na kipa wa villa kuucheza.
Kikosi cha Yanga SC kilikuwa: Ally Mustaph, Juma Abdul, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Nadir Haroub/Pato Ngonyani dk71, Mbuyu Twite/Andrey Coutinho dk89, Deus Kaseke, Salum Telela, Amis Tambwe/Simon Msuva dk77, Malimi Busungu/Kpah Sherman dk70 na Godfrey Mwashiuya.
SC Villa: Sebwato Nicolaus, Khamis Katende/Mboa Paul dk69, Wasibi Yesiri, Katongwe Henry, Mugabi Jonathan, Luanga Thedeo, Kasule Abdulkarim/Edua Abeid dk55, Lansana Kamara, Kasumba Omary, Achema Rober na Kasabant James.


MSUVA AWAPA SARE YA 0 - 0 YANGA KWA KUPAISHA PENALTI, 


Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM

MABINGWA wa Tanzania Bara, Yanga SC jioni ya leo wamelazimishwa sare ya bila kufungana na SC Villa ya Uganda katika mchezo wa kirafiki, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga SC watajilaumu wenyewe kwa sare hiyo, kwani walipata nafasi kadhaa za kufunga ikiwemo penalti, iliyopaishwa na mchezaji bora wa Ligi Kuu, Simon Msuva dakika za lala salama.
Timu hizo zilianza kushambuliana kwa zamu, huku zote zikicheza soka maridadi ya utulivu na pasi za uhakika kabla ya dakika ya 27 Kasumba Omary wa Villa nusura kumzunguka Nahodha wa Yanga SC, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ lakini beki wa kulia Oscar Joshua akaondosha mpira kwenye hatari.
Dakika ya 28 Achema Robert alipiga shuti kali likatoka nje, kabla ya shuti lake lingine kudakwa na kipa wa Yanga SC, Ally Mustafa ‘Barthez’ dakika ya 33.
Malimi Busungu wa Yanga SC alipiga nje dakika ya 32 kufuatia pasi nzuri ya Amisi Tambwe. Busungu tena dakika ya 35 alimdakisha kipa wa Villa, Sebwato Nicolaus baada ya kupiga ndani ya boksi.
Tambwe naye alipoteza nafasi ya kufunga dakika ya 34 baada ya shuti lake kudakwa na kipa wa Villa, Sebweto.
Katika mchezo huo, Kocha mpya wa Simba Dylan Kerr aliingia kuwatazama wapinzani, kipindi cha pili Yanga SC walitengeneza nafasi nzuri, lakini wakashindwa kutumia.
Dakika ya 50 Deus Kaseke aligongesha mwamba, dakika ya 54 krosi nzuri ya Juma Abdul ilidakwa na kipa wa Villa, Sebwato.
Yanga SC ilipata pigo dakika ya 71, baada ya Nahodha wake, Cannavaro kuumia juu ya jicho na kushindwa kuendelea na mchezo, nafasi yake ikichukuliwa na Pato Ngonyani aliyekwenda kucheza vizuri.
Winga mpya machachari wa Yanga SC, Godfrey Mwashiuya aliunganisha vizuri krosi ya Kpah Sherman dakika ya 76, lakini beki wa Villa, Wasibi akaokoa mpira ukiwa unaelekea nyavuni.
Msuva akapaisha penalti dakika ya 78 baada ya kipa wa Villa kumuangusha Kaseke kwenye eneo la hatari na dakika ya 80 Mwashiuya aliipiga shuti maridadi lililookoleea na kipa wa villa kuucheza.
Kikosi cha Yanga SC kilikuwa: Ally Mustaph, Juma Abdul, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Nadir Haroub/Pato Ngonyani dk71, Mbuyu Twite/Andrey Coutinho dk89, Deus Kaseke, Salum Telela, Amis Tambwe/Simon Msuva dk77, Malimi Busungu/Kpah Sherman dk70 na Godfrey Mwashiuya.
SC Villa: Sebwato Nicolaus, Khamis Katende/Mboa Paul dk69, Wasibi Yesiri, Katongwe Henry, Mugabi Jonathan, Luanga Thedeo, Kasule Abdulkarim/Edua Abeid dk55, Lansana Kamara, Kasumba Omary, Achema Rober na Kasabant James.





Ghana FA kukanusha ubadhirifu Brazil


Ghana FA lakanusha ubadhirifu Brazil
Shirikisho la soka la Ghana GFA limekanusha madai ya ubadhirifu wa fedha katika kombe la dunia la Brazil 2014.
Shirikisho hilo limeitupia tope ripoti ya kamati maalum iliyoundwa kutathmini sababu za matokeo duni huko Brazil 2014.
''Kamati ya Dzamefe'' ilichapisha ripoti yake majuzi na ikaonesha kuwa mpakuaji mipira wa timu ya Black Stars alilipwa kiasi sawa cha fedha na Washambuliaji Asamoah Gyan na hata kocha wa timu ya taifa James Kwesi Appiah.
null
Meza ya michezo ya BBC ndiyo iliyopasua mbarika kuwa Hamidu alilipwa pesa sawa na kocha na wachezaji nyota .
Ripoti hiyo ilionesha kuwa yule msaidizi anayeokota mipira na kupanga jezi za timu ya taifa alilipwa takriban dola laki moja $100,000.
Ismail Hamidu alipokea pesa hizo japo GFA inailaumu kamati hiyo kwa kuidunisha kazi yake.
Meza ya michezo ya BBC ndiyo iliyopasua mbarika kuwa Hamidu alilipwa pesa sawa na kocha na wachezaji nyota .
null
Sasa GFA imewataka mawakili wake wawasilishe kesi mahakamani kupinga kuchafuliwa jina
Kamati hiyo vilevile inasema kuwa kunakiasi kikubwa tu cha pesa zilizopewa GFA ambazo hazijabainika zilipo.
Sasa GFA imewataka mawakili wake wawasilishe kesi mahakamani kupinga kuchafuliwa jina.
Ghana ilishindwa kufuzu kwa mkondo wa pili huko Brazil licha ya serikali kutuma zaidi ya dola milioni 3 pesa taslimu kupelekwa Brazil ilikuzima mgomo wa wachezaji waliokuwa wakilalamikia malimbikizi ya marupurupu yao.


Tevez arejea  Boca Juniors


Straika wa Argentina Carlos Tevez amekamilisha Uhamisho wake kwenda Boca Juniors kutoka kwa Mabingwa wa Italy Juventus.
Tevez, mwenye Miaka 31, alianzia Soka lake huko kwao na Klabu ya Boca ambayo aliihama Mwaka 2004 kwenda Brazil kuchezea Corinthians na kisha kukaa Miaka 9 akichezea Klabu za Ulaya.
Huko Ulaya alizichezea Klabu za England, West Ham, Mwaka 2006-2007, Manchester United, 2007-2009, na Manchester City, 2009-2013, na kisha kwenda Italy kuichezea Juventus ambako msimu uliopita aliisaidia tena kutetea Taji lao la Ubingwa kwa kupiga Bao 20.
Majuzi Juventus walimbadili Tevez kwa kumsaini Straika wa Atletico Madrid ya Spain, Mario Mandzukic ambae anatoka Croatia.
Akithibitisha Uhamisho huu, Rais wa Boca Juniors Daniel Angelici alisema: "Ni Siku ya furaha sana na ya kuridhisha. Kurudi kwa Tevez akiwa kwenye kilele cha mafanikio ni habari njema kwa Washirika na Mashabiki wote wa Boca na Soka la Argentina!"

Alhamisi, 25 Juni 2015

Southgate kuendelea kuwa kocha England


MKUDE NAYE KWA NGASA BONDENI!

Mkude anakwenda kufanya majaribio katika klabu ya Bidvets ya Afrika Kusini.
Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema uongozi umempa ruksa na tayari umezungumza na uongozi wa benchi la ufundi la Taifa Stars.
“Tumemumbeaoa ruhusa Mkude aende kwenye majaribio, kwa kuwa amechaguliwa timu ya taifa, nao tumewasiliana nao.
“Kocha Mkwasa ni kati ya watu ambao wangependa maendeleo ya wachezaji kwenda nje, hii pia itaisaidia Taifa Stars. Hivyo hawezi kuwa na tatizo,” alisema.
Majaribio yanaweza kuwa ya wiki moja hadi zaidi kulingana na mahitaji ya timu hiyo inayomilikiwa na moja ya vyuo vikuu vikongwe barani Afrika cha Wits cha jijini Johannesburg.

MKWASA AOMBA ASIPIGWE MAWE SIMBA

Katika mazungumzo hayo Mkwasa amesema kuna mambo ambayo Watanzania tunapaswa kuyapa nafasi katika Timu ya Taifa.
Kwanza lilikuwa ni lile la kuwapa nafasi vijana wa kikosi chake kwa kuwa ndiyo wanaanza kujipanga.
“Wavumilieni kwa kuwa sasa ndiyo wanajipanga upya tena. Waungeni mkono na msitumie muda mwingi kuwazoemea au kuwapiga.
“Nafikiri hatuko katika hali ambayo tunaweza kusema tumekaa vizuri, tunahitaji kujipanga. Tafadhari tupeni muda,” alisema Mkwasa.
Lakini la pili ni lile ambalo wakati anazungumza, aliwagusa na Simba.
“Nitapita hadi kwenda mazoezi ya baadhi ya timu kwa ajili ya kuangalia wachezaji. Lengo ni kupata wale wenye kiwango chenye msaada.
“Ninaweza kuzungumza na makocha wa timu mbalimbali pia. Mfano naweza kuwatembelea mazoezini na kushauriana nao.
KAIJAGE AWAOMBA WACHEZAJI TANZANITE KURIPOTI KAMBINI KUJIANDAA DHIDI YA ZAMBIA




Timu ya taifa ya soka ya Wanawake 'Tanzanite' wenye umri chini ya miaka 20 (U-20) Tanzanite Stars, imeingia kambini jana jioni Mbande jijini Dar es salaam na itakua ikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.

Kikosi cha wacheaji 22 chini ya Kocha Mkuu, Rogasian Kaijage kinafanya mazoezi asubuhi na jioni katika uwnaja wa Azam uliopo Chamazi kujiandaa na mchezo dhidi ya U-20 ya Zambia utakaofanyika kati ya Julai 10, 11 na 12 jijini Dar es salaam.

Mchezo huo dhidi ya Zambia ni wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Wanawake za Dunia wenye umri chini ya miaka ya 20, zitakazofanyika nchini Papua New Guinea mwaka 2016.

Wachezaji waliopo kambini ni, NajiAati Abbasi, Zuwena Aziz, Shelder Boniface, Stumai Abdallah, Donisia Daniel, Tatu Iddy (Evergreen Queens), Niwael  Khalfani, Maimuna Hamis (Mburahati Queens), Anastazia Anthony, Amisa Athumani, Amina Ramadhani, Neem Paulo (JKT Queens).

Wengine ni Asha Shaban, Rebeka Daniel, Brandina Wincelaus (Tanga), Happines Hezroni, Jane Cloudy (JKT Queens), Wema Richard, Gerwa Lugomba, Sadda Ramadhani (Uzuri Queens), Anna Hebron (Evergreen Queens) na Shehati Mohamed (Mburahati Queens)

Aidha wachezaji Monica Henry, Tumaini Michael (Uzuri Queens), Diana Msewa (Mbeya), na Vailet Nicolaus (Evergreen) bado hawajaripoti kambini wanaombwa kuripoti  na kuungana na wenzao katika maandalizi ya mchezo huo dhidi ya Zambia.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


chanzo saleh jembe

Jumatatu, 22 Juni 2015

Man U yamwinda Schweinsteiger na Ramos


Scweinsteiger
Klabu ya Manchester United ina hamu ya kumsajili kiungo wa kati wa Bayern Bastian Schweinsteiger na mlinzi wa Real Madrid Sergio Ramos.
Kocha wa klabu hiyo Louis Van Gaal anajaribu kuimarisha kikosi chake baada ya kumaliza katika nafasi nne katika jedwali la ligi ya EPL.
null
Sergio Ramos
Schweinsteiger mwenye umri wa miaka 30 na Ramos mwenye umri wa miaka 29 ni kati ya wale wanaomvutia.
Kandarasi ya Ramos itakamilika mwaka 2017 huku ile ya Schweinsteiger ikiendelea hadi mwisho wa mwaka 2016.

chanzo(bbc swahili.com)

Ripoti ya Gaza:Pande zote zilikiuka haki

  • Saa moja iliyopita
Vita vya Gaza
Ripoti iliyosubiriwa na wengi, imeonyesha kuwepo na ushahidi wa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu pamoja na sheria ya kimataifa kutoka kwa pande zote.
Israel imepuzilia mbali ripoti hiyo na kuitaja kama inayochochewa kisiasa.
Vita hivyo vilisalia kwa siku 50 na kumalizika kwa mkataba wa amani.
Kwa upande wa Palestina watu 2,251, zaidi ya elfu moja wakiwa ni raia waliuawa.
null
Vita vya Gaza
Upande wa Israel uliwapoteza wanajeshi 67 wakiwemo raia sita.
Israel imejitetea na kusema ilianzisha operesheni dhidi ya Gaza ili kuzima mashambulio ya roketi yaliyokua yakirushwa na makundi ya wapiganaji, ambayo yalichimba mahandaki kutekeleza mashambulizi.
Ripoti hii ya tume ya haki za binadamu katika Umoja wa Mataifa ilikumbwa na mzozo tangu mwanzo.
Mkuu wa uchunguzi alilazimika kujiondoa bada ya Israel kulalamika kwamba alikuwa na uwonevu.
null
Vita vya Gaza
Aidha alituhumiwa kuwahi kufanya kazi na chama cha ukombozi wa Palestina PLO.
Israel ilikataa kushirikiana na uchunguzi kwa madai kwamba tayari ilikua imehukumiwa tangu mwanzo