Mechi za klabu bingwa barani Ulaya katika hatua ya robo fainali ziliendelea tena usiku wa kuamkia leo kwa michezo miwili kupigwa. Bayern Munich walikuwa ugenini kukipiga na FC Porto ya Ureno. Katika hali isiyotarajiwa na wengi Bayern imeangukia pua kwa kucharazwa mabao 3-1.
Nako nchini Ufaransa wenyeji Paris Saint German ilishuka dimbani kuikabili miamba ya soka ya Hispania Barcelona. Katika mchezo huo wenyeji PSG wamejiweka katika hali ngumu baada ya kucharazwa mabao 3-1. Bao la Neymar jr na mawili ya Luis Suárez yalitosha kuwazamisha wenyeji wao na kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.
Timu zote nne zitacheza michezo ya marudiano April 21 siku ya Jumanne.
Kocha wa Dortmund kubwaga manyanga.
Kocha Jurgen Klopp wa Borrusia Dortmund
Kocha wa klabu ya soka ya Ujerumani Borrusia Dortmund Jurgen Klopp amesema atasitisha mkataba wake na timu hiyo mwishoni mwa msimu huu. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 47, ameomba kukatisha mkataba huo ambao ulipaswa kumalizika mwaka 2018. ‘’ Si hivyo bali nimechoka, sijafanya mawasiliano na timu yoyote na sifikirii kuchukua likizo isiyo na malipo” alisema Klopp.
Kocha huyo ameifundisha Dortmund tangu mwaka 2008 huku akifanikiwa kutwaa mataji mawili ya ligi ya nchi hiyo pamoja na kutinga fainali klabu bingwa Ulaya mwaka 2012-13, japokuwa msimu huu wanaonekana kupepesuka katika msimamo wa ligi ambapo mpaka sasa wapo nafasi ya kumi huku utofauti wa point kati yao na vinara wa ligi hiyo Bayern Munich ikiwa ni point 37.
Majeruhi Yanga kuikabili Etoile du Sahel
Andrey Coutinho
Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Mbrazil Andrey Coutinho huenda akawa sehemu ya mchezo kati ya klabu yake na Etoile du Sahel ya Tunisia katika mechi ya Shirikisho Afrika hapo Jumamosi jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa daktari wa timu hiyo, Juma Sufiani, majeruhi wa Yanga, akiwemo Jerryson Tegete na Salum Telela wanaendelea vizuri na kucheza au kutocheza itakuwa ni maamuzi ya kocha.
Yanga inaendelea na mazoezi Da es Salaam kujiandaa na mechi hiyo ya kwanza.
Etoile du Sahel ya Tunisia inategemewa kuwasili Dar es Salaam Alhamisi kwa ajili ya mechi hiyo na watafanya mazoezi Ijumaa katika uwanja wa Taifa kujiweka tayari na mchezo huo.
Mechi ya marudiano itachezwa Tunis, Tunisia baada ya wiki mbili.
Azam yaipa Yanga ya ubingwa
Yanga kwa raha zao
Kicheko kinaendelea kutawala katika klabu ya Yanga baada ya sare kuendelea kuitesa Azam FC katika mechi ya tatu mfululizo hivyo kuipa Yanga nafasi ya ubingwa.
Azam , katika mechi ya leo iliyochezwa mkwakwani mjini Tanga, imetoka droo ya 0-0 na wenyeji Mgambo Shooting.
Katika mechi iliyopita, mabingwa hao watetezi walitoka sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar, ikiwa ni juma moja tu baada ya kutoka sare ya 1-1 na Mbeya City.
Sare hizo zinaipa Yanga nafasi ya ubingwa kwa tofauti ya pointi 7.
Kocha was Yanga, Hans Pluijm amenukuliwa name vyombo vya habari akisema, anahitaji mechi tano tu kushinda ili kuwa mabingwa.
Yanga, ikiwa na kibarua cha mechi ya Shirikisho barani Afrika dhidi ya Etoile du Sahel ya Tunisia hapo Jumamosi jijini Dar es Salaam, inaongoza ligi ikiwa na pointi 46 katika mechi 21 ilizocheza wakati Azam inafuatia ikiwa na pointi 39.
Logo hiyo inaelekea ukingoni kuisha hapo mwezi Mei
Maoni 1 :
yanga msipo shinda kaz kwen mwendapo tunixsia
Chapisha Maoni