Jumapili, 8 Januari 2017

4G NDANI YA ZANZIBAR , AZAMU 4 YANGA 0




Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva amesema wamekikubali kipigo kutoka Azam FC lakini bado wana nafasi ya kujirekebisha.

Yanga imepokea kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa Azam FC katika mechi ya mwisho ya Kundi B katika michuano ya Mapinduzi. Mechi hiyo imechezwa jana kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Msuva amesema mashabiki wasikate tamaa, waendelee kuwaunga mkono nao kupitia benchi la ufundi na wao wenyewe watajirekebisha.

"Mpira una matokeo matatu, kushinda, sare au kufungwa. Kufungwa imetutokea sisi, lakini hatuna ujanja. Nawaomba mashabiki wasikate tamaa na badala yake waendelee kutuunga mkono.

"Benchi la ufundi wameona makosa yetu, sisi wachezaji tumeona na tutayafanyia kazi na kuendelea kufanya vizuri.

"Unajua kikubwa ambacho ni kizuri tumevuka kwenda nusu fainali hivyo tuna nafasi ya kujirekebisha kwenye nusu fainali na ikiwezekana fainali," alisema.






Baada ya Yanga kupoteza kwa mabao 4-0 dhidi ya Azam FC, Simba imesema itaendelea kuchukua tahadhari kubwa kwa kila mechi yake ya Kombe la Mapinduzi.

Simba imeshinda mechi zake zote za Mapinduzi lakini haikuwa ikishinda kwa idadi kubwa ya mabao kama ilivyo kwa Yanga.

Simba inashuka dimbani Amaan mjini Zanzibar kuivaa Jang’ombe Boys katika michuano hiyo.

Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja amesema wako tayari na wanachotaka ni kufanya vizuri.

“Kila mechi ni mechi nyingine, lazima kuwa makini kwa lengo la kufanya vizuri,” alisema.

Simba inaongoza Kundi A ikiwa na pointi saba baada ya kushinda mbili na sare moja.


Iwapo itashinda leo, uhakika asilimia mia kuivaa Yanga katika nusu fainali utakuwa umepatikana.
 
SOURCE SALEHJEMBE


Jumanne, 3 Januari 2017


Baada ya Coastal Union kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 4–1 dhidi ya Kimondo FC kwenye Uwanja wa Karume jijini  Dar, kocha wa timu hiyo, Mohamed Kampira ameibuka na kusema anatamani mechi zao zote za nyumbani zilizosalia wamalizie uwanjani hapo.


Mchezo huo wa Kundi B, ulipangwa kuchezwa uwanjani hapo ikiwemo ni sehemu ya adhabu kwa Coastal Union kucheza mechi moja nje ya uwanja wao wa nyumbani wa Mkwakwani na mbili kucheza hapo bila ya mashabiki baada ya mashabiki wake kumpiga mwamuzi walipocheza dhidi ya KMC.

Kocha huyo alidai kuwa, wanapocheza nje ya Mkwakwani ndiyo wanacheza vizuri zaidi na kupata matokeo mazuri tofauti na wanapocheza nyumbani.

“Tangu msimu huu uanze, hatujawahi kushinda wala kupata sare katika uwanja wetu wa nyumbani, tumefungwa na Polisi Morogoro, KMC na Njombe Mji, lakini tukicheza nje ya tunapata matokeo mazuri.

“Nadhani uwanja wetu wa nyumbani tunafanya vibaya  kutokana na presha ya mashabiki wetu kutaka matokeo ya haraka kiasi cha kusababisha wachezaji kushindwa  kucheza kwa kufuata maelekezo, hivyo ni bora mechi zetu zote za nyumbani tuchezee katika Uwanja wa Karume, Dar,” alisema Kampira.

Coastal Union kwa sasa inashika nafasi ya sita ikiwa na pointi tisa, huku KMC ikiongoza kundi hilo ikiwa na ponti 19.

SOURCE SALEHJEMBE





Zikiwa zimebaki wiki mbili pekee kabla ya kuanza kwa Michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (Afcon), beki wa Yanga aliye na kikosi cha timu ya taifa ya Togo, Vincent Bossou ameweka bayana kwamba atapigana kwenye kombe hilo kuhakikisha kwamba anaitangaza timu yake.

Bossou ni miongoni mwa wachezaji watatu watakaoiwakilisha Ligi ya Tanzania Bara kwenye mashindano hayo yatakayofanyika nchini Gabon kuanzia Januari 14 wengine ni Bruce Kangwa wa Azam na Juuko Murshid wa Simba ambapo Togo imepangwa kundi C, ikiwa na timu za Morocco, Ivory Coast na DR Congo.

Akizungumza kutoka Senegal kilipo kikosi hicho kwenye kambi yake amesema kwamba:

“Nipo huku Senegal kabla ya kwenda Gabon kushiriki Afcon, niwaambie mashabiki wa Yanga na Tanzania kwa ujumla kuwa nimepanga kuonyesha kiwango kama nilivyokuwa huko kwa ajili ya kuitangaza ligi ya Bongo watu wanifuatilie waone moto wangu.


“Najua hilo nitalifanikisha kwa sababu nipo vizuri na bado nina kiwango kilekile nilipokuwa huko na tunaamini kwamba tunaweza kufanya vizuri katika mashindano haya kwa sababu tuna kikosi kizuri licha ya kwamba tupo kwenye kundi gumu,”alisema Bossou.

SOURCE: CHAMPIONI