Alhamisi, 5 Mei 2016

MUM VETERANI YAKUBALI KICHAPO NYUMBAN



Timu ya wachezaji wakongwe wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro(MUM VETERANI) imeendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu baada ya kukubali kipigo kingine kutoka kwa Young Muslim ya mkoani hapa.

Timu hiyo inayoundwa na wachezaji wa zamani wa timu ya Chuo Kikuu cha Wislam cha Morogoro ilikubali kipigo cha 2-0 nyumbani dhidi ya wageni Young Muslim ambao walionekana kutawala kwa asilimia kubwa mchezo huo.

Jamal Sarah ndiye alikuwa wa kwanza kutikisa nyavu za wenyeji baada ya kuiandikia Young Muslim goli la kwanza kabla ya Said Abdallah kutikisa tena nyavu hizo nakuipatia timu yake goli la pili na kufanya mambo yabaki hivyo mpaka mwisho wa mchezo huo.

Mara baada ya mchezo huo Msimamizi wa timu ya Young Muslim Ashraf Suleiman(pedo) aliipongeza timu yake kwa kupata ushindi huo wa ugenini licha ya kukiri kwamba bado timu yake inahitaji marekebisho.

“bado tunahitaji mabadiliko makubwa katika safu yetu ya ushambuliaji na kiungo ili kuwa na kasi zaidi ya mashamblizi na ufungaji magoli” Alisema Suleiman(pedo).

Timu ya Young Muslim inayomilikiwa na Ashraf Suleiman(pedo) ipo katika maandalizi kwa ajiri ya kushiriki ligi daraja la nne mkoani Morogoro ambapo mchezo dhidi ya MUM VETERAN ni sehemu ya maandalizi hayo.




MUM VETERANI FC wakiwa katika picha ya pamoja.  pincha na Majid Yusuf

Timu ya Young Muslim ikipasha kabla ya mechi yao na MUM VETERANI FC .  pincha na Majid Yusuf


Timu ya Young Muslim ikipokea maelekezo kutoka kwa kiongozi wake Ashraf Suleimani( Pedo).  pincha na Majid Yusuf


Timu ya Young Muslim ikiwa katika picha ya pamoja .  pincha na Majid Yusuf


Timu ya wachezaji wakongwe wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro(MUM VETERANI) imeendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu baada ya kukubali kipigo kingine kutoka kwa Young Muslim ya mkoani hapa.

Timu hiyo inayoundwa na wachezaji wa zamani wa timu ya Chuo Kikuu cha Wislam cha Morogoro ilikubali kipigo cha 2-0 nyumbani dhidi ya wageni Young Muslim ambao walionekana kutawala kwa asilimia kubwa mchezo huo.

Jamal Sarah ndiye alikuwa wa kwanza kutikisa nyavu za wenyeji baada ya kuiandikia Young Muslim goli la kwanza kabla ya Said Abdallah kutikisa tena nyavu hizo nakuipatia timu yake goli la pili na kufanya mambo yabaki hivyo mpaka mwisho wa mchezo huo.

Mara baada ya mchezo huo Msimamizi wa timu ya Young Muslim Ashraf Suleiman(pedo) aliipongeza timu yake kwa kupata ushindi huo wa ugenini licha ya kukiri kwamba bado timu yake inahitaji marekebisho.

“bado tunahitaji mabadiliko makubwa katika safu yetu ya ushambuliaji na kiungo ili kuwa na kasi zaidi ya mashamblizi na ufungaji magoli” Alisema Suleiman(pedo).

Timu ya Young Muslim inayomilikiwa na Ashraf Suleiman(pedo) ipo katika maandalizi kwa ajiri ya kushiriki ligi daraja la nne mkoani Morogoro ambapo mchezo dhidi ya MUM VETERAN ni sehemu ya maandalizi hayo.







Timu za MUM VETERANI FC na Young Muslim wakipongezana baada ya kumaliza mchezo wao wa kirafiki.  pincha na Majid Yusuf


Young Muslim fc na MUM VETERANI FC wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mchezo wao wa kirafiki wakidumisha amani na mshikamano. pincha na Majid Yusuf

Hakuna maoni: