BALOTELLI SASA MIAKA 25, ASHEREKEA NA JEZI YAKE YA ITALIA
Mshambuliaji mwenye
vituko wa Liverpool, Mario Balotelli amesherekea siku yake ya kuzaliwa kwa
kuwaalika wachezaji wenzake.
Balotelli
aliamua kutengeneza keki yenye jezi namba 9 ambayo huivaa anapokuwa timu ya
taifa ya Italia na si ile anayovaa Liverpool.
Ni mwaka wa 25
sasa kwake, na wachezaji walijitokeza katika mgahawa wa Sorrento kuungana naye,
baadhi wakiwa na familia zao.
Kati ya
walioungana na Balotelli ni pamoja na Lucas Leiva, Mamadou Sakho, Lazar
Markovic, Roberto Firmino, Divock Origi, Emre Can, Dejan Lovren na Martin
Skrtel.
MAN CITY YAINGIA KWENYE VITA YA KUZING'OA MAN UNITED, ARSENAL KWA PEDRO, BENZEMA
Wakati Manchester United wako katika juhudi kuu
kuhakikisha wanambasa Pedro Rodriguez wa Barcelona, wapinzani wao wakubwa Manchester
City nao wameingia vitani.
Man City wameingia vitani wakitaka kumpata nyota huyo
huku kukiwa na taarifa nyingine pia wanamhitaji Karim Benzema ambaye anatakiwa
na Arsenal.
Tayari Pedro amesema anaweza kuondoka Barcelona kwa
kuwa inaonekana haelewani na Kocha Louis Enrique lakini uamuzi wa City kuanza
kumfuatilia unaamsha vita mpya kabisa.
Tayari Man United iko tayari kutoa pauni milioni 22
kumpata, kuingia kwa City kunaweza kusababisha kupanda kwa bei ya kiungo huyo
mwenye miaka 28.
Man United inataka kumchukua kwa lengo kuziba nafasi
ya Angel Di Maria ambaye amekwenda PSG.
Pedro ndiye alikuwa shujaa wa Barcelona baada ya
kufunga bao lililoipa Barcelona ubingwa wa Uefa Super Cup kwa kuichapa Sevilla
kwa mabao 5-4.
MESSI KIBOKO YA SEVILLA, MECHI 24 AMEPIGA MABAO 24
Lionel Messi
ni kiboko, yale mabao mawili aliyofunga dhidi ya Sevilla katika fainali ya Uefa
Super Cup yamempafanya afikishe mabao 24 katika mechi 24 dhidi ya timu hiyo.
Hapo
unajumlisha pia mechi za La Liga na Copa de Rey. Huyu mtu ni hatari!
Ukiachana
na hivyo, Sevilla inakuwa timu ya pili kufungwa mabao 24 katika mechi 24, Messi
pia ameifanyia hivyo Atletico Madrid.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni