Jumatano, 1 Julai 2015

 

Julai 18, 2015 KMKM vs Telecom            APR  Vs  Shandy                Yanga Vs Gor Mahia        Julai 19, 2015 LLB AFC Vs Hegaan FC   Adama City Vs Malaika Azam Vs KCCA                  Julai 7, 2015 Telecom Vs Khartoum  Gor Mahia Vs KMKM  Julai 21, 2015 Shandy Vs LLB AFC       Hegaan Vs  APR    Malaika Vs Azam         Julai 22, 2015 Khartoum Vs KMKM KCCA Vs Adama City Telecom Vs Yanga     Julai 23, 2015 Hegaan Vs Shandy APR Vs LLB AFC      Julai 24, 2015 Khartoum Vs Gor Mahia KMKM Vs Yanga Julai 25, 2015 KCCA Vs Malakia Adama City Vs Azam     Julai 26, 2015 Gor Mahia Vs Telecom     Yanga Vs Khartoum      Julai 27, 2015 MAPUMZIKO Julai 28, 2015 ROBO FAINALI B1 Vs A3 A1 Vs Mshindi wa tatu Bora Julai 29, 2015 B2 Vs C2 C1 Vs A2 Julai 29, 2015 MAPUMZIKO Julai 31, 2015 NUSU FAINALI Mshindi 25 Vs Mshindi 26 Mshindi 23 Vs Mshindi 24 Agosti 1, 2015 MAPUMZIKO Agosti 2, 2015  MSHINDI WA TATU NA FAINALI Aliyefungwa 27 Vs Aliyefungwa 28 Mshindi 27 Vs Mshindi 28

 

 

 FRIENDS RANGERS BAADA YA KUJIPIMA NA YANGA , YAWAFATA AZAM CHAMANZI COMPLEX KESHO "


azam (1)Kikosi cha timu ya Friends Rangers, kesho asubuhi kinashuka kwenye Uwanja wa Azam Complex, uliopo Chamazi Dar es Salaam, kuvaana na timu ya Azam FC, katika mchezo wakirafiki.
Afisa habari wa klabu hiyo Asha Kigundula alisema kuwa, mchezo huo utafanyika asubuhi kuanzia saa 2, asubuhi.
Kigundula alisema kuwa wameshukuru kupata mechi hiyo ambayo itaendelea kuiweka timu yao katika mazingira mazuri kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi daraja la kwanza.
Alisema kuwa kucheza na timu kama Azam ni sehemu nzuri ya kukipa kikosi chao mazoezi mazuri, kwa sababu Azam ni timu bora na inawachezaji wenye uwezo mkubwa hapa nchini.
Kigundula alisema tayari kikosi chao kimeshacheza mechi mbili za kirafiki, dhidi ya Yanga ambapo ilifungwa mabao 3-2, mchezo uliyofanyika kwenye Uwanja wa Karume, Ilala Dar es Salaam.
Mechi nyingine ambayo Friends Rangers ilicheza na timu ya Mwadui FC, timu hiyo ya Magomeni Kagera ilishinda kwa mabao 2-1.

Chanzo, shafiidauda.blogspot.com


Mkuu wa Mkoa wa Manyara Dokta, Joel Bendera ameipongezs TFF kwa kuandaa mashindano ya ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 13 (U-13),  na maandalizi ya timu hiyo kwa ajili ya kuwania kufuzu kwa fainali za Afrika za vijana chini ya miaka 17 zitakazofanyika mwaka 2019 nchini Tanzania.

Bendera amesema hiyo ndiyo njia sahihi ya kuelekea kwenye mafanikio pia amepongeza juhudi za Chama cha Soka mkoa wa Manyara na TFF kwa kuandaa kozi za makocha na waamuzi, akisema huo ndiyo uwekezaji mkubwa katika maendeleo ya soka mkoani Manyara.
Aidha aliwaasa makocha kutumia mbinu za kisasa za ufundishaji soka walizozipata kwenda kuendeleza vipaji vya wachezaji watakaowafundisha.
Pia Bendera amewahakikishia wakazi wa Manyara atahakikisha wanaandaa vipaji vitakvyowawezesha kuwa na timu bora itakayowakilisha mkoa wa Manyara.

 

KLABU ya TP Mazembe imethibitisha kupokea ofa ya klabu ya Lille ya Ufaransa kumtaka Nahodha wa Zambia, Rainford Kalaba (pichani kulia). Mwenyekiti wa Mazembe, Moise Katumbi amesema kwamba mabingwa hao wa Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo (DRC) wanaitathmini ofa ya Lille kwa Kalaba. Kalaba amekuwa akihusishwa na mpango wa kuhamia Lille, kufuatia kocha wa zamani wa Zambia, Herve Renard kuteuliwa kuwa Kocha Mkuu wa klabu hiyo Ligi Kuu nchini humo, maarufu kama Ligue One Mei mwaka huu. “Lille inamtaka Kalaba aende huko na tupo kwenye mazungumzo juu ya safari ya Lille,” amesema Katumbi. “Sasa tatizo ni tunataka mustakabali mzuri kwa Kalaba. Tunatazama hilo kama Kalaba atakwenda huko ili mradi tu au kwa mustakabali mzuri. “Unatakiwa kuangalia mustakabali na ada ya uhamsho kwa Kalaba, kwa sababu unajua mchezaji anapotoka Afrika wanatoa fedha kidogo na hiyo ndiyo inayoziua timu nyingi (kwa Afrika).” Kalaba amekuwa mchezaji wa Mazembe tangu mwaka 2010 alipojiunga na timu hiyo ya Lubumbashi yenye washambuliaji wawili Watanzania, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu kwa mkopo kutoka Sporting Braga ya Ureno, kabla ya kusaini Mkataba wa moja kwa moja mwishoni mwa msimu wake wa kwanza DRC. Kiungo huyo wa Zambia alikuwa mfungaji bora wa Mazembe msimu wa 2013/2014 kwa mabao yake tisa, akiisaidia timu ya Lubumbashi kubeba taji la nne mfululizo na la 14 la Ligi ya DRC.

 

 

Murray kucheza raundi ya pili Wimbledon

Andy Murray mcheza tenis wa Uingereza afuzu raundi ya pili ya michuano ya tenis ya Wimbledon 2015
Andy Murray anaungana na Waingereza wenzake watatu kucheza hatua ya pili ya michuano ya tenis ya Wimbledon inayoendelea jijini London, baada ya kumcharaza Mikhail Kukushkin wa Kazakhstan.
Murray, wa tatu kwa ubora duniani alishinda kwa seti 6-4 7-6 (7-3) 6-4 katika mchezo uliodumu kwa saa mbili na dakika 13 wakati hali ya hewa ikiwa nyuzi joto 41 za Selisyasi.
Murray anasema ilikuwa mechi ngumu. Na yeye ndiye aliyeifanya iwe hivyo katika seti ya pili ya mchezo.
Kuingia raundi ya pili Murray anaungana na Waingereza wenzake Liam Broady, Aljaz Bedene na James Ward kutinga raundi ya pili, akiwemo pia Heather Watson namba moja kwa ubora nchini Uingereza kwa upande wa wanawake akimbwaga Caroline Garcia wa Ufaransa kwa seti 1-6 6-3 8-6 .
Hii ni mara ya kwanza kwa Waingereza wanne kwa pamoja kutinga raundi ya pili tangu mwaka 2006. Katika raundi hiyo Murray atakabiliana na Mholanzi Robin Haase, ambaye alimbandua Alejandro Falla wa Colombia kwa seti nne.


Hakuna maoni: