Alhamisi, 4 Juni 2015

 

 


Kikosi kingine cha timu ya Taifa kitaondoka nchini siku ya jumamosi kuelekea nchini Rwanda kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya Rwanda katika kumbukumbu ya mauaji ya Kimbali.

Kocha Salum Mayanga ataondoka na kikosi cha wachezaji 18 kuelekea nchini Rwanda kwa ajili ya mchezo huo wa kirafiki, akisaidiwa na kocha Bakari Shime.
Wachezaji watakaondoka kwenda Rwanda ni Peter Manyika, Said Mohamed, Emmanuel Semwanda, Joram Mgeveke, Hassan Isihaka, Gadiel Michael, Hassan Dilunga, Rashid Mandawa, Atupele Green, Kelvin Friday, Hassan Kessy, Ibrahim Hajibu, Malimi Busungu, Mudathir Yahya, Deus Kaseke, Andre Vicent, Amri Kiemba na Mohamed Hussein.


Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Mart Nooij ametangaza kikosi cha wachezaji 23 kilichoondoka jana jioni kwenda Addis Ababa nchini Ethiopia kuweka kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo dhidi ya Misri.

Msafara wa Taifa Stars utaongozwa na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji, Vedastus Lufano na Geofrey Irick Nyange “Kaburu” ambaye pia ni Makamu Rais wa klabu ya Simba.
Mchezo kati ya Misri na Tanzania unatarajiwa kuchezwa Juni 14, katika uwanja wa Borg El Arab jijini Alexandria, ikiwa ni mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa Afrika (AFCON) mwaka  2017.
 
Kikosi cha Stars kiliondoka saa 11 jioni kwa Shirika la ndege la Ethiopia ambapo inatarajiwa kuwasili jiji la Addis Ababa majira ya saa 1 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Wachezaji wanaosafiri kuelekea nchini Ethiopia ni  Deogratias Munish, Aishi Manula, Mwadini Ali, walinzi Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Erasto Nyoni, Nadir Haroub, Aggrey Morris, Mwinyi Haji, Salum Mbonde na Juma Abdul.
Wengine ni Mwinyi Kazimoto, Abdi Banda, Salum Telela, Frank Domayo, Jonas Mkude, Said Ndemla, washambuliaji Saimon Msuva, John Bocco, Thomas Ulimwengu, Mbwana Samatta,Mrisho Ngasa na Juma Liuzio.

Naye mjumbe wa kamati ya Utendaji  ya TFF Vedastus Lufano amesema timu inakwenda kuweka kambi Ethiopia kwa ajili ya kupambana katika mchezo dhidi ya Misri.

Afisa wa FIFA akiri alipokea mrungula!

 

Chuck Blazer
Wizara ya Sheria ya Marekani imechapisha taarifa inayoelezea jinsi Afisa wa zamani wa FIFA Chuck Blazer alivyokiri kuwa yeye pamoja na wenzake walipokea rushwa ikiwa ni pamoja kuichagua Afrika Kusini kuwa mwenyeji wa fainali ya kombe la dunia mwaka 2010.
Katika taarifa hiyo imeweka wazi mtandao wa malipo ya rushwa ulivyokuwa ukifanywa ndani ya shirikisho la soka duniani FIFA, taarifa zinazoegemea uchunguzi uliofanywa na shirika la kijasusi la Marekani FBI.
Taarifa hiyo ambayo inamwelezea Afisa humo wa zamani wa Fifa Chuck Blazer kukiri kupokea rushwa sasa huenda ikaibua mengi kwenye kashfa ya rushwa inayoindamana shirikisho la FIFA.
Mmerakani huyo kwenye taarifa hiyo inadai alikuwa ni mmoja wa watu waliosuka mipango ya kupokea rushwa katika tukio jingine la fainali la kombe la dunia 1998.
Taarifa za Kukiri zipo katika maandishi wakati wa kesi yake mwaka 2013 wakati kesi yake ilipokuwa akisikilizwa katika mahakama ya Easten New York huko Marekani ambapo alikiri makosa kumi yaliyokuwa yanamkabili.
Blazer alikuwa afisa wa ngazi juu wa FIFA eneo la kanda ya Amerika Kaskazini na Kati na ukanda wa nchi Caribbean kuanzia mwaka 1990 hadi mwaka 2011.
Marekani imefungua kesi ya rushwa inayowakabili maafisa wa FIFA jambo lililofanya Rais wa FIFA Sepp Blatter kuamua kutangaza kujiuzulu.
Mwendesha mashtaka wa Marekani wiki iliyopita aliwashtaki maafisa 14 wa ngazi wa juu wa FIFA tuhuma za rushwa, kutakatisha fesha,

Afrika Kusini yakana kutoa hongo kwa FIFA

        Afrika kusini
Afrika kusini imekana kwa mara nyengine tena kwamba ilitoa hongo ili kupewa maandalizi ya kombe la dunia la mwaka 2010.
Waziri wa michezo nchini humo Fikile Mbalula, amewaambia wanahabari kwamba Afrika kusini itashirikiana na wachunguzi kutoka Marekani lakini imekataa kuingizwa katikati ya ugomvi kati ya FIFA na Marekani.
Amesema kuwa dola millioni 10 zilizotolewa zilikuwa malipo ya kusaidia soka miongoni mwa raia wa Afrika wanaoishi katika visiwa vya Caribbean na yalilipwa miaka kadhaa baada ya michuano hiyo kuandaliwa na Afrika kusini.

 

Benitez ndio kocha mpya wa Real Madrid

Rafa Benitez ndio mkufunzi mpya wa Real Madrid
Aliyekuwa kocha wa Napoli Rafa Benitez amethibitishwa kuwa k ocha wa Real Madrid katika kandarasi ya miaka mitatu.
Benitez mwenye umri wa miaka 55 anachukua mahala pake Carlo Ancelotti ambaye aliondoka katika kilabu hiyo miezi 12 tu baada ya kuisaidia kushinda kombe lao la kumi la vilabu bingwa Ulaya.
Benitez ambaye ni mzaliwa wa Madrid amehudumu misimu miwili kama mkufunzi wa Napoli ,baada kufanikiwa na vilabu kadhaa vya Ulaya.
Baada ya kuisaidia Valencia kushinda kombe la Uefa mwaka 2004,mwaka unaofuatia alielekea Liverpool na kuisaidia kilabu hiyo kushinda kombe la vilabu bingwa ikiwa ni msimu wake wa kwanza katika kilabu hiyo ya Mersyside.
Miaka miwili baadaye aliisaidia Liverpool kufika katika fainali za kombe la vilabu bingwa Ulaya na mwaka 2013 alikuwa kaimu mkufunzi wa Chelsea waliposhinda kombe la Yuropa.

Hakuna maoni: