Jumanne, 19 Mei 2015

 

Cosafa Cup | RESULTS


18 May
 
Tanzania0 - 1Swaziland
Olympia Park Stadium
18 May
 
Lesotho1 - 2Madagascar
Olympia Park Stadium

17 May
 
Zimbabwe2 - 0Mauritius
Carlos Rusere (28)
Ronald Chitiyo (66)

 
Moruleng Stadium


17 May
 
Namibia0 - 0Seychelles
Moruleng Stadium

SAMATTA, ULIMWENGU SASA WABEBA MATUMAINI YA NOOIJ TAIFA STARS


RATIBA YA MECHI ZA KUNDI G

Jumamosi Juni 13, 2015
Nigeria v Chad
Misri v Tanzania
Jumamosi Sept 5, 2015
Tanzania v Nigeria
Chad v Misri
Ijumaa Machi 25, 2016
Chad v Tanzania
Nigeria v Misri
Jumatatu Machi 28, 2016
Tanzania v Chad
Misri v Nigeria
Jumamosi Juni 4, 2016
Chad v Nigeria
Tanzania v Misri
Jumamosi Sept 3, 2016
Nigeria v Tanzania
Misri v Chad
  Kutoka RUSTENBURG
KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mholanzi, Mart Nooij amesema kwamba anatarajia washambuliaji wa TP Mazembe ya DRC, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu watakiongezea kikosi chake kwa ajili ya mechi za kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika.
 

Nooij anasema hayo baada ya Stars jana kupoteza mchezo wake wa kwanza wa Kombe la COSAFA dhidi ya Swaziland.
 

Amesema anashukuru kwa kupata mwaliko wa kushiriki COSAFA, kwani kwake anatumia michuano hii kama sehemu ya maandalizi ya kuwania kufuzu AFCON na CHAN Juni.
 

Amesema anaamini wachezaji aliowaacha majeruhi nyumbani pamoja na nyota hao wa TP Mazembe, watakiongeza nguvu katika kikosi chake kitakaporejea Tanzania.
Amesema amepoteza mchezo wa kwanza COSAFA ambao alitarajia kushinda, lakini vijana walicheza vizuri kipindi cha kwanza, kabla bao la wapinzani kuwapoteza mchezoni.
 

“Presha ya mchezo ilikua kubwa hasa kipindi cha pili, kutokana na vijana wangu kucheza kwa kusaka bao, huku Swaziland wakimiliki zaidi mpira na kukuta mipango yetu kutokua na madhara” alisema Nooij.
 

Nooij ameiongoza Stars katika mechi ya 14 jana tangu awasili mwishoni mwa Aprili kuchukua mikoba ya Mdenmark, Kim Poulsen na timu hiyo imefungwa bao 1-0 na Swaziland katika mchezo wa kwanza wa Kundi B Kombe la COSAFA Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace mjini hapa.
 

Katika mechi 14 ambazo Nooij ameiongoza Stars, imeshinda tatu tu, ikifungwa tano na kutoa sare mara sita, tena mechi nyingi ikicheza nyumbani.
 

Matokeo hayo yanaiweka Stars katika mazingira magumu ya kwenda Robo Fainali- baada ya Madagascar kuifunga 2-1 Lesotho katika mchezo wa kwanza.
Stars sasa lazima ishinde mechi zake mbili zijazo dhidi ya Lesotho na Madagascar



Swaziland ambayo bao lake pekee lilifungwa na  Sifiso Mabila kwa shuti kali dakika ya 42 baada ya kutanguliziwa pasi kwenye njia na Xolani Sibandze aliyemtoka Oscar Joshua upande wa kushoto, waliizidi ufundi uwanjani Stars jana.
 

Taifa Stars itatupa kete yake ya pili kesho Saa 11:00 jioni kwa saa za Afrika kusini, sawa na Saa 12:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki dhidi ya Madagascar katika Uwanja wa Royal Bafokeng. Madagascar walishinda mabao 2-1 dhidi ya Lesotho katika mchezo wa kwanza jana.
 

Baada ya COSAFA, Taifa Stars inatarajiwa kwenda kuweka kambi Addis Ababa, Ethiopia mwezi ujao kujiandaa na mchezo wa kwanza wa Kundi G dhidi ya Misri, kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika 2017 nchini Gabon.
 
 

 

NOOIJ AKALIA KUTI KAVU TAIFA STARS, MECHI 14 TIMU IMESHINDA TATU TU TANGU ATUE APRILI


KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mholanzi Mart Nooij anaweza kufukuzwa wakati wowote kuanzia sasa, kufuatia idadi kubwa ya Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutomkubali.
 

Nooij ameiongoza Stars katika mechi ya 14 jana tangu awasili mwishoni mwa Aprili kuchukua mikoba ya Mdenmark, Kim Poulsen na timu hiyo imefungwa bao 1-0 na Swaziland katika mchezo wa kwanza wa Kundi B Kombe la COSAFA Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace mjini hapo.
 

Matokeo hayo yanaiweka Stars katika mazingira magumu ya kwenda Robo Fainali- baada ya Madagascar kuifunga 2-1 Lesotho katika mchezo wa kwanza.
 

Stars sasa lazima ishinde mechi zake mbili zijazo dhidi ya Lesotho na Madagascar ili kuangalia uwezekano wa kwenda Robo Fainali.
 

Swaziland ambayo bao lake pekee lilifungwa na  Sifiso Mabila kwa shuti kali dakika ya 42 baada ya kutanguliziwa pasi kwenye njia na Xolani Sibandze aliyemtoka Oscar Joshua upande wa kushoto, waliizidi ufundi uwanjani Stars jana.
 

Stars ilicheza ovyo jana, mpango pekee wa kutafuta mabao ni kwa mipira ya kutokea pembeni, wakati huo huo timu ilitumia mshambuliaji mmoja tu, John Bocco ambaye muda mwingi alikuwa anakwenda kutafuta mipira pembeni.
Ilikuwa vigumu kuelewa Stars wanacheza mfumo gani jana, kwani pamoja na kuwa na viungo watatu uwanjani, Erasto Nyoni, Mwinyi Kazimoto na Said Ndemla, lakini bado timu ilikuwa haikai na mpira.
 

Mipira yote ilikuwa inapelekwa pembeni kwa mawinga akina Mrisho Ngassa na Simon Msuva wakampigie krosi Bocco aliyedhibitiwa vizuri na mabeki wa Swaziland.
 

Hali ilikuwa mbaya zaidi kipindi cha pili, kwani Stars haikurudi na mpango mbadala- matokeo yake Swaziland wakang’ara zaidi uwanjani.
 

Mabadiliko yaliyofanywa na Nooij kipindi cha pili, yalikuwa kichekesho pia- kwani baada ya dakika 10 kipindi cha pili, Stars ilionekana kabisa ilihitaji kiungo mbadala wa Mwinyi Kazimoto, lakini Mholanzi huyo alimtoa Said Ndemla na kumuingiza Juma Luizio dakika ya 65. 
 

Maana yake alipunguza kiungo akaongeza mshambuliaji, lakini dakika 10 baadaye akapunguza tena mshambuliaji, Mrisho Ngassa na aliyeonekana kuwa muhimu zaidi uwanjani jana na kuingiza kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
 

Mtu ambaye alitakiwa kumbadili mapema tu, pengine tangu mwanzoni mwa kipindi cha pili, Simon Msuva akamtoa mwishioni mwa mchezo dakika ya 82 akimuingiza Ibrahim Hajibu.
 

Pamoja na mapungufu ya wachezaji kutokana na nyota kadhaa wa timu hiyo kubaki Dar es Salaam kwa sababu mbalimbali, ikiwemo majeruhi, lakini hata upangaji wa timu Nooij pia ulikuwa ni tatizo.
 

Bado kutoka wachezaji aliokuja nao hapa, angeweza kupanga timu tofauti na aliyopanga jana na ikacheza kwa uelewano mzuri na kupata matokeo mazuri.
 

Wajumbe kadhaa wa Kamati ya Utendaji wa TFF wanaamini Stars haipo katika mikono salama kwa Nooij na wanataka mabadiliko mapema kabla ya kuanza kwa kampeni za kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika Juni.
 

Kuna wasiwasi hata juu ya mbinu za ufundishaji wa Nooij na ndiyo maana amekuwa hataki hata Waandishi wa Habari wa Tanzania wahudhurie mazoezi yake wala kupiga picha.
 

Mfumo pekee wa kushambulia anaofundisha mazoezini na kiungo kupeleka pasi pembeni, imkute winga apige krosi watu ‘wagombee goli’ na ndivyo hata Stars inavyoonekana kucheza sasa.
 

Utamu wa soka ya Taifa Stars umepungua kwa kiasi kikubwa kutoka ulivyokuwa chini ya kocha aliyetangulia, Kim Poulsen hadi Nooij na mchezo wa kesho wa COSAFA dhidi ya Madagascar unaweza kuamua hatima ya Mholanzi huyo.
 

Ingawa kuna imani kwamba, Nooij anapotoshwa na mtu wake wa karibu katika uteuzi wa wachezaji, lakini hata yeye mwenyewe kama kocha ni tatizo.
 

Katika mechi 14 ambazo Nooij ameiongoza Stars, imeshinda tatu tu, ikifungwa tano na kutoa sare mara sita, tena mechi nyingi ikicheza nyumbani.
 

TFF ilihadaika na wasifu mzuri wa Nooij aliyetua Tanzania akitokea klabu ya St George ya Ethiopia Aprili mwaka jana na kumpa Mkataba mnono. 
 

Wasifu wa Nooij unasema amewahi kuwa mwalimu maalum katika programu za maendeleo ya soka katika Chama cha Soka Uholanzi (DFA) na pia amewahi kufundisha timu ya EVC 1913 ya Marekani na baadaye Kazakhstan.
 

Alikuwa kocha wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Burkina Faso katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2003 na mwaka 2004 alikuwa kocha wa muda wa klabu ya FC Volendam ya Uholanzi.
 

Mwaka 2007 aliteuliwa kuwa kocha wa Msumbiji na akaiwezesha kufuzu kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2010, hiyo ikiwa ni mara ya kwanza Mambas wanashiriki AFCON baada ya msoto wa miaka 12.
 
 
Hata hivyo, katika fainali hizo, Msumbiji ilishika mkia katika kundi lake baada ya kuambulia sare moja na kufungwa mechi mbili. Baada ya kukosa tiketi ya AFCON 2012, Nooij akajiuzulu Septemba mwaka 2011 na nafasi yake kuchukuliwa na Mjerumani, Gert Engels.
 

Aprili 19 mwaka 2012, aliajiriwa na klabu ya Santos ya Afrika Kusini, ambako hata hivyo alifukuzwa Desemba 18, mwaka 2012 na kuhamia St George ya Ethiopia kabla ya kuja Tanzania Aprili mwaka jana. 
 
 
 
REKODI YA MART NOOIJ TAIFA STARS
Tanzania 0-0 Malawi (Kirafiki Mbeya)
Tanzania 1-0 Zimbabwe (kufuzu AFCON Dar es Salaam)
Tanzania 1-0 Malawi (kirafiki Taifa)
Tanzania 2-2 Zimbabwe (Kufuzu AFCON Harare)
Tanzania 2-4 Botswana (kirafiki Harare)
Tanzania 2-2 Msumbiji (Kufuzu AFCON Dar es Salaam)
Tanzania 1-2 Msumbiji (Kufuzu AFCON Maputo)
Tanzania 0-2 Burundi (Kirafiki, Bujumbura)
Tanzania 4-1 Benin (Kirafiki, Dar es Salaam)
Tanzania 1-1 Swaziland (Kirafiki, Mbabane)
Tanzania 1-2 Burundi (Kirafiki, Taifa. Stars Maboresho)
Tanzania 1-1 Rwanda (kirafiki Mwanza, Maboresho)
Tanzania 1-1 Malawi  (Kirafiki Mwanza, Stars kubwa)

 

 

West Brom waikalisha Chelsea 3-0

West Brom imewachabanga mabingwa ligi kuu ya England Chelsea jumla ya mabao 3-0 hali ambayo kwa sasa inaifanya klabu hiyo kukaa eneo salama zaidi dhidi ya kushuka daraja.

Katika mechi hiyo iliyochezwa, dimba la The Hawthons, Saido Berahino alikata utepe wa magoli kwa kufunga goli la kwanza mnamo dakika ya 9,na pia dakika ya 47 Berahino tena akaweka kimiani goli la pili kwa njia ya penati ,baada ya kuangushwa na John Terry eneo la adhabu na hivyo hadi mwisho wa mchezo West Brom 3 Chelsea mabingwa nunge.
 Kwa matokeo hayo West Brom sasa wamefanikiwa kukaa eneo salama kuepuka kushuka daraja,huku Chelsea wakiwa bado mabingwa. Kesho Arsenal watakwaana na Sunderland.


Raheem Sterling kuipa kisogo Liverpool?


Raheem Sterling wa Liverpool anatarajia kumuaga kocha wa klabu hiyo Brendan Rodgers na kuondoka Anfield msimu huu.

Mshambuliaji huyo katika ligi ya England tayari amekwisha saini mkataba mwingine wa kiasi cha Paund laki moja kwa wiki na kukanusha kuwa yeye hana tamaa na pesa,kama alivyohojiwa nabaadhi ya vyombo vya habari.

Mchezaji huyo anatarajiwa kukutana na Mkurugenzi wake Ian Ayre na Kocha wake Rodgers siku ya ijumaa,ambapo atakuwa tayari kuwaeleza kuwa sasa anapaswa kuiipa kisogo klabu hiyo.

Hata hivyo klabu hiyo ya Liverpool haijataka kusema lolote kwa sasa japo kuwa inaeleweka kuwa bado wanamhitaji mchezaji huyo kinda mwenye umri wa miaka 20 na ambaye mkataba wake unaisha mwaka 2017.

Klabu kadhaa zimeonyesha nia ya kumsajili mchezaji huyo, ikiwemo Manchester City,Arsenal pamoja na timu nyingine kubwa Ulaya zinamhitaji pia. 

Hata hivyo Kaptain wa Liverpool Steven Gerrard akizungumza sikuya Ijumaa wiki iliyopita alimtaka Sterling kubakia katika timu hiyo na kusisitiza kuwa ni vizuri kuwa katika klabu ambayo kocha ana imani na wewe.

 

NYOTA MPYA MAN UNITED ABEBA KIATU CHA DHAHABU UHOLANZI

MSHAMBULIAJI wa PSV, Memphis Depay amethibitishwa kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Uholanzi, maarufu kama Eredivisie baada ya mechi za mwisho za ligi hiyo Jumapili. 
 
Kinda huyo wa umri wa miaka 21, ambaye amekubali kujiunga na Manchester United msimu ujao kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 25, amefunga mabao 22 katika mechi 30 alizocheza, na kuwa mchezaji mdogo zaidi kutwaa tuzo hiyo tangu mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Ronaldo mwaka 1995.
 
Depay amekuwa na mchango mkubwa kwa PSV kutwaa taji la ligi ya Uholanzi msimu huu, kikosi cha kocha Phillip Cocu kikiwazidi kwa pointi 17 Ajax walioshika nafasi ya pili. Walimalizia msimu kwa ushindi wa 3-2 ugenini dhidi ya ADO Den Haag.
 

English Barclays Premier League | LOGS

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Chelsea37259370313984
2Manchester City37237781384376
3Arsenal36218767353271
4Manchester United37209862372569
5Liverpool37188115142962
6Tottenham Hotspur37187125753461
7Southampton371861354312360
8Swansea City37168134648-256
9Stoke City37149144244-251
10Everton371211144849-147
11West Ham United371211144445-147
12Crystal Palace37129164651-545
13West Bromwich Albion371111153747-1044
14Leicester City37108194154-1338
15Aston Villa37108193156-2538
16Sunderland36716133050-2037
17Newcastle United3799193863-2536
18Hull City37810193351-1834
19Burnley37612192753-2630
20Queens Park Rangers3786234168-2730
 
 

Spanish La Liga | LOGS

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Barcelona373034108198993
2Real Madrid372926111357689
3Atletico de Madrid37238667293877
4Valencia CF372111567303774
5Sevilla37227868432573
6Villarreal371612948331560
7Athletic Club371410133841-352
8Malaga37148154045-550
9Espanyol371310144548-349
10Rayo Vallecano37154184464-2049
11Celta de Vigo371212134442248
12Real Sociedad371013144049-943
13Elche37117193562-2740
14Getafe37107203057-2737
15Levante3799193467-3336
16Granada CF37713172964-3534
17Deportivo de La Coruna37713173358-2534
18Eibar3788213155-2432
19Almeria3788213361-2832
20Cordoba37311232265-4320

 

Hakuna maoni: