Cosafa Cup | RESULTS
|
| ||||||||||||||||||||||||||
|
|
SAMATTA, ULIMWENGU SASA WABEBA MATUMAINI YA NOOIJ TAIFA STARS
Kutoka RUSTENBURG
KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mholanzi, Mart Nooij amesema kwamba anatarajia washambuliaji wa TP Mazembe ya DRC, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu watakiongezea kikosi chake kwa ajili ya mechi za kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika.
KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mholanzi, Mart Nooij amesema kwamba anatarajia washambuliaji wa TP Mazembe ya DRC, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu watakiongezea kikosi chake kwa ajili ya mechi za kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika.
Nooij anasema hayo baada ya Stars jana kupoteza mchezo wake wa kwanza wa Kombe la COSAFA dhidi ya Swaziland.
Amesema anashukuru kwa kupata mwaliko wa kushiriki COSAFA, kwani kwake anatumia michuano hii kama sehemu ya maandalizi ya kuwania kufuzu AFCON na CHAN Juni.
Amesema anaamini wachezaji aliowaacha majeruhi nyumbani pamoja na nyota hao wa TP Mazembe, watakiongeza nguvu katika kikosi chake kitakaporejea Tanzania.
Amesema amepoteza mchezo wa kwanza COSAFA ambao alitarajia kushinda, lakini vijana walicheza vizuri kipindi cha kwanza, kabla bao la wapinzani kuwapoteza mchezoni.
“Presha ya mchezo ilikua kubwa hasa kipindi cha pili, kutokana na vijana wangu kucheza kwa kusaka bao, huku Swaziland wakimiliki zaidi mpira na kukuta mipango yetu kutokua na madhara” alisema Nooij.
Nooij ameiongoza Stars katika mechi ya 14 jana tangu awasili mwishoni mwa Aprili kuchukua mikoba ya Mdenmark, Kim Poulsen na timu hiyo imefungwa bao 1-0 na Swaziland katika mchezo wa kwanza wa Kundi B Kombe la COSAFA Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace mjini hapa.
Katika mechi 14 ambazo Nooij ameiongoza Stars, imeshinda tatu tu, ikifungwa tano na kutoa sare mara sita, tena mechi nyingi ikicheza nyumbani.
Matokeo hayo yanaiweka Stars katika mazingira magumu ya kwenda Robo Fainali- baada ya Madagascar kuifunga 2-1 Lesotho katika mchezo wa kwanza.
Stars sasa lazima ishinde mechi zake mbili zijazo dhidi ya Lesotho na Madagascar
Swaziland ambayo bao lake pekee lilifungwa na Sifiso Mabila kwa shuti kali dakika ya 42 baada ya kutanguliziwa pasi kwenye njia na Xolani Sibandze aliyemtoka Oscar Joshua upande wa kushoto, waliizidi ufundi uwanjani Stars jana.
Taifa Stars itatupa kete yake ya pili kesho Saa 11:00 jioni kwa saa za Afrika kusini, sawa na Saa 12:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki dhidi ya Madagascar katika Uwanja wa Royal Bafokeng. Madagascar walishinda mabao 2-1 dhidi ya Lesotho katika mchezo wa kwanza jana.
Baada ya COSAFA, Taifa Stars inatarajiwa kwenda kuweka kambi Addis Ababa, Ethiopia mwezi ujao kujiandaa na mchezo wa kwanza wa Kundi G dhidi ya Misri, kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika 2017 nchini Gabon.
NOOIJ AKALIA KUTI KAVU TAIFA STARS, MECHI 14 TIMU IMESHINDA TATU TU TANGU ATUE APRILI
KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mholanzi Mart Nooij anaweza kufukuzwa wakati wowote kuanzia sasa, kufuatia idadi kubwa ya Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutomkubali.
Nooij ameiongoza Stars katika mechi ya 14 jana tangu awasili mwishoni mwa Aprili kuchukua mikoba ya Mdenmark, Kim Poulsen na timu hiyo imefungwa bao 1-0 na Swaziland katika mchezo wa kwanza wa Kundi B Kombe la COSAFA Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace mjini hapo.
Matokeo hayo yanaiweka Stars katika mazingira magumu ya kwenda Robo Fainali- baada ya Madagascar kuifunga 2-1 Lesotho katika mchezo wa kwanza.
Stars sasa lazima ishinde mechi zake mbili zijazo dhidi ya Lesotho na Madagascar ili kuangalia uwezekano wa kwenda Robo Fainali.
Swaziland ambayo bao lake pekee lilifungwa na Sifiso Mabila kwa shuti kali dakika ya 42 baada ya kutanguliziwa pasi kwenye njia na Xolani Sibandze aliyemtoka Oscar Joshua upande wa kushoto, waliizidi ufundi uwanjani Stars jana.
Stars ilicheza ovyo jana, mpango pekee wa kutafuta mabao ni kwa mipira ya kutokea pembeni, wakati huo huo timu ilitumia mshambuliaji mmoja tu, John Bocco ambaye muda mwingi alikuwa anakwenda kutafuta mipira pembeni.
Ilikuwa vigumu kuelewa Stars wanacheza mfumo gani jana, kwani pamoja na kuwa na viungo watatu uwanjani, Erasto Nyoni, Mwinyi Kazimoto na Said Ndemla, lakini bado timu ilikuwa haikai na mpira.
Mipira yote ilikuwa inapelekwa pembeni kwa mawinga akina Mrisho Ngassa na Simon Msuva wakampigie krosi Bocco aliyedhibitiwa vizuri na mabeki wa Swaziland.
Hali ilikuwa mbaya zaidi kipindi cha pili, kwani Stars haikurudi na mpango mbadala- matokeo yake Swaziland wakang’ara zaidi uwanjani.
Mabadiliko yaliyofanywa na Nooij kipindi cha pili, yalikuwa kichekesho pia- kwani baada ya dakika 10 kipindi cha pili, Stars ilionekana kabisa ilihitaji kiungo mbadala wa Mwinyi Kazimoto, lakini Mholanzi huyo alimtoa Said Ndemla na kumuingiza Juma Luizio dakika ya 65.
Maana yake alipunguza kiungo akaongeza mshambuliaji, lakini dakika 10 baadaye akapunguza tena mshambuliaji, Mrisho Ngassa na aliyeonekana kuwa muhimu zaidi uwanjani jana na kuingiza kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
Mtu ambaye alitakiwa kumbadili mapema tu, pengine tangu mwanzoni mwa kipindi cha pili, Simon Msuva akamtoa mwishioni mwa mchezo dakika ya 82 akimuingiza Ibrahim Hajibu.
Pamoja na mapungufu ya wachezaji kutokana na nyota kadhaa wa timu hiyo kubaki Dar es Salaam kwa sababu mbalimbali, ikiwemo majeruhi, lakini hata upangaji wa timu Nooij pia ulikuwa ni tatizo.
Bado kutoka wachezaji aliokuja nao hapa, angeweza kupanga timu tofauti na aliyopanga jana na ikacheza kwa uelewano mzuri na kupata matokeo mazuri.
Wajumbe kadhaa wa Kamati ya Utendaji wa TFF wanaamini Stars haipo katika mikono salama kwa Nooij na wanataka mabadiliko mapema kabla ya kuanza kwa kampeni za kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika Juni.
Kuna wasiwasi hata juu ya mbinu za ufundishaji wa Nooij na ndiyo maana amekuwa hataki hata Waandishi wa Habari wa Tanzania wahudhurie mazoezi yake wala kupiga picha.
Mfumo pekee wa kushambulia anaofundisha mazoezini na kiungo kupeleka pasi pembeni, imkute winga apige krosi watu ‘wagombee goli’ na ndivyo hata Stars inavyoonekana kucheza sasa.
Utamu wa soka ya Taifa Stars umepungua kwa kiasi kikubwa kutoka ulivyokuwa chini ya kocha aliyetangulia, Kim Poulsen hadi Nooij na mchezo wa kesho wa COSAFA dhidi ya Madagascar unaweza kuamua hatima ya Mholanzi huyo.
Ingawa kuna imani kwamba, Nooij anapotoshwa na mtu wake wa karibu katika uteuzi wa wachezaji, lakini hata yeye mwenyewe kama kocha ni tatizo.
Katika mechi 14 ambazo Nooij ameiongoza Stars, imeshinda tatu tu, ikifungwa tano na kutoa sare mara sita, tena mechi nyingi ikicheza nyumbani.
TFF ilihadaika na wasifu mzuri wa Nooij aliyetua Tanzania akitokea klabu ya St George ya Ethiopia Aprili mwaka jana na kumpa Mkataba mnono.
Wasifu wa Nooij unasema amewahi kuwa mwalimu maalum katika programu za maendeleo ya soka katika Chama cha Soka Uholanzi (DFA) na pia amewahi kufundisha timu ya EVC 1913 ya Marekani na baadaye Kazakhstan.
Alikuwa kocha wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Burkina Faso katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2003 na mwaka 2004 alikuwa kocha wa muda wa klabu ya FC Volendam ya Uholanzi.
Mwaka 2007 aliteuliwa kuwa kocha wa Msumbiji na akaiwezesha kufuzu kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2010, hiyo ikiwa ni mara ya kwanza Mambas wanashiriki AFCON baada ya msoto wa miaka 12.
Hata hivyo, katika fainali hizo, Msumbiji ilishika mkia katika kundi lake baada ya kuambulia sare moja na kufungwa mechi mbili. Baada ya kukosa tiketi ya AFCON 2012, Nooij akajiuzulu Septemba mwaka 2011 na nafasi yake kuchukuliwa na Mjerumani, Gert Engels.
Aprili 19 mwaka 2012, aliajiriwa na klabu ya Santos ya Afrika Kusini, ambako hata hivyo alifukuzwa Desemba 18, mwaka 2012 na kuhamia St George ya Ethiopia kabla ya kuja Tanzania Aprili mwaka jana.
REKODI YA MART NOOIJ TAIFA STARS
Tanzania 0-0 Malawi (Kirafiki Mbeya)
Tanzania 1-0 Zimbabwe (kufuzu AFCON Dar es Salaam)
Tanzania 1-0 Malawi (kirafiki Taifa)
Tanzania 2-2 Zimbabwe (Kufuzu AFCON Harare)
Tanzania 2-4 Botswana (kirafiki Harare)
Tanzania 2-2 Msumbiji (Kufuzu AFCON Dar es Salaam)
Tanzania 1-2 Msumbiji (Kufuzu AFCON Maputo)
Tanzania 0-2 Burundi (Kirafiki, Bujumbura)
Tanzania 4-1 Benin (Kirafiki, Dar es Salaam)
Tanzania 1-1 Swaziland (Kirafiki, Mbabane)
Tanzania 1-2 Burundi (Kirafiki, Taifa. Stars Maboresho)
Tanzania 1-1 Rwanda (kirafiki Mwanza, Maboresho)
Tanzania 1-1 Malawi (Kirafiki Mwanza, Stars kubwa)
West Brom waikalisha Chelsea 3-0
West
Brom imewachabanga mabingwa ligi kuu ya England Chelsea jumla ya mabao
3-0 hali ambayo kwa sasa inaifanya klabu hiyo kukaa eneo salama zaidi
dhidi ya kushuka daraja.
Katika mechi hiyo iliyochezwa, dimba la
The Hawthons, Saido Berahino alikata utepe wa magoli kwa kufunga goli la
kwanza mnamo dakika ya 9,na pia dakika ya 47 Berahino tena akaweka
kimiani goli la pili kwa njia ya penati ,baada ya kuangushwa na John
Terry eneo la adhabu na hivyo hadi mwisho wa mchezo West Brom 3 Chelsea
mabingwa nunge.
Kwa matokeo hayo West Brom sasa wamefanikiwa kukaa eneo
salama kuepuka kushuka daraja,huku Chelsea wakiwa bado mabingwa. Kesho
Arsenal watakwaana na Sunderland.
Raheem Sterling kuipa kisogo Liverpool?
Raheem Sterling wa Liverpool anatarajia kumuaga kocha wa klabu hiyo Brendan Rodgers na kuondoka Anfield msimu huu.
Mshambuliaji
huyo katika ligi ya England tayari amekwisha saini mkataba mwingine wa
kiasi cha Paund laki moja kwa wiki na kukanusha kuwa yeye hana tamaa na
pesa,kama alivyohojiwa nabaadhi ya vyombo vya habari.
Mchezaji huyo anatarajiwa kukutana
na Mkurugenzi wake Ian Ayre na Kocha wake Rodgers siku ya ijumaa,ambapo
atakuwa tayari kuwaeleza kuwa sasa anapaswa kuiipa kisogo klabu hiyo.
Hata
hivyo klabu hiyo ya Liverpool haijataka kusema lolote kwa sasa japo
kuwa inaeleweka kuwa bado wanamhitaji mchezaji huyo kinda mwenye umri wa
miaka 20 na ambaye mkataba wake unaisha mwaka 2017.
Klabu kadhaa
zimeonyesha nia ya kumsajili mchezaji huyo, ikiwemo Manchester
City,Arsenal pamoja na timu nyingine kubwa Ulaya zinamhitaji pia.
Hata
hivyo Kaptain wa Liverpool Steven Gerrard akizungumza sikuya Ijumaa
wiki iliyopita alimtaka Sterling kubakia katika timu hiyo na kusisitiza
kuwa ni vizuri kuwa katika klabu ambayo kocha ana imani na wewe.
NYOTA MPYA MAN UNITED ABEBA KIATU CHA DHAHABU UHOLANZI
MSHAMBULIAJI
wa PSV, Memphis Depay amethibitishwa kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu ya
Uholanzi, maarufu kama Eredivisie baada ya mechi za mwisho za ligi hiyo
Jumapili.
Kinda
huyo wa umri wa miaka 21, ambaye amekubali kujiunga na Manchester
United msimu ujao kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 25, amefunga
mabao 22 katika mechi 30 alizocheza, na kuwa mchezaji mdogo zaidi kutwaa
tuzo hiyo tangu mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Ronaldo
mwaka 1995.
Depay
amekuwa na mchango mkubwa kwa PSV kutwaa taji la ligi ya Uholanzi msimu
huu, kikosi cha kocha Phillip Cocu kikiwazidi kwa pointi 17 Ajax
walioshika nafasi ya pili. Walimalizia msimu kwa ushindi wa 3-2 ugenini
dhidi ya ADO Den Haag.
English Barclays Premier League | LOGS
Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
1 | Chelsea | 37 | 25 | 9 | 3 | 70 | 31 | 39 | 84 |
2 | Manchester City | 37 | 23 | 7 | 7 | 81 | 38 | 43 | 76 |
3 | Arsenal | 36 | 21 | 8 | 7 | 67 | 35 | 32 | 71 |
4 | Manchester United | 37 | 20 | 9 | 8 | 62 | 37 | 25 | 69 |
5 | Liverpool | 37 | 18 | 8 | 11 | 51 | 42 | 9 | 62 |
6 | Tottenham Hotspur | 37 | 18 | 7 | 12 | 57 | 53 | 4 | 61 |
7 | Southampton | 37 | 18 | 6 | 13 | 54 | 31 | 23 | 60 |
8 | Swansea City | 37 | 16 | 8 | 13 | 46 | 48 | -2 | 56 |
9 | Stoke City | 37 | 14 | 9 | 14 | 42 | 44 | -2 | 51 |
10 | Everton | 37 | 12 | 11 | 14 | 48 | 49 | -1 | 47 |
11 | West Ham United | 37 | 12 | 11 | 14 | 44 | 45 | -1 | 47 |
12 | Crystal Palace | 37 | 12 | 9 | 16 | 46 | 51 | -5 | 45 |
13 | West Bromwich Albion | 37 | 11 | 11 | 15 | 37 | 47 | -10 | 44 |
14 | Leicester City | 37 | 10 | 8 | 19 | 41 | 54 | -13 | 38 |
15 | Aston Villa | 37 | 10 | 8 | 19 | 31 | 56 | -25 | 38 |
16 | Sunderland | 36 | 7 | 16 | 13 | 30 | 50 | -20 | 37 |
17 | Newcastle United | 37 | 9 | 9 | 19 | 38 | 63 | -25 | 36 |
18 | Hull City | 37 | 8 | 10 | 19 | 33 | 51 | -18 | 34 |
19 | Burnley | 37 | 6 | 12 | 19 | 27 | 53 | -26 | 30 |
20 | Queens Park Rangers | 37 | 8 | 6 | 23 | 41 | 68 | -27 | 30 |
Spanish La Liga | LOGS
Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
1 | Barcelona | 37 | 30 | 3 | 4 | 108 | 19 | 89 | 93 |
2 | Real Madrid | 37 | 29 | 2 | 6 | 111 | 35 | 76 | 89 |
3 | Atletico de Madrid | 37 | 23 | 8 | 6 | 67 | 29 | 38 | 77 |
4 | Valencia CF | 37 | 21 | 11 | 5 | 67 | 30 | 37 | 74 |
5 | Sevilla | 37 | 22 | 7 | 8 | 68 | 43 | 25 | 73 |
6 | Villarreal | 37 | 16 | 12 | 9 | 48 | 33 | 15 | 60 |
7 | Athletic Club | 37 | 14 | 10 | 13 | 38 | 41 | -3 | 52 |
8 | Malaga | 37 | 14 | 8 | 15 | 40 | 45 | -5 | 50 |
9 | Espanyol | 37 | 13 | 10 | 14 | 45 | 48 | -3 | 49 |
10 | Rayo Vallecano | 37 | 15 | 4 | 18 | 44 | 64 | -20 | 49 |
11 | Celta de Vigo | 37 | 12 | 12 | 13 | 44 | 42 | 2 | 48 |
12 | Real Sociedad | 37 | 10 | 13 | 14 | 40 | 49 | -9 | 43 |
13 | Elche | 37 | 11 | 7 | 19 | 35 | 62 | -27 | 40 |
14 | Getafe | 37 | 10 | 7 | 20 | 30 | 57 | -27 | 37 |
15 | Levante | 37 | 9 | 9 | 19 | 34 | 67 | -33 | 36 |
16 | Granada CF | 37 | 7 | 13 | 17 | 29 | 64 | -35 | 34 |
17 | Deportivo de La Coruna | 37 | 7 | 13 | 17 | 33 | 58 | -25 | 34 |
18 | Eibar | 37 | 8 | 8 | 21 | 31 | 55 | -24 | 32 |
19 | Almeria | 37 | 8 | 8 | 21 | 33 | 61 | -28 | 32 |
20 | Cordoba | 37 | 3 | 11 | 23 | 22 | 65 | -43 | 20 |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni